logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wema Sepetu: “Nimekata Tamaa, Kwa Umri Wangu Sina Imani Ya Kupata Mtoto!”

“Kwa umri wangu sasa miaka 35, safari yangu ya kutafuta mtoto pia imefika mwisho. Hata ile hamu haipo, umefika wakati nimekata tamaa,” Sepetu alisema kwa kujisikitikia.

image
na MOSES SAGWE

Burudani20 January 2025 - 14:25

Muhtasari


  • Wema alisema kwamba kwa umri aliofikia, yeye atabakia tu ku’adopt mbwa na kuwalea, akisema kwamba yeye anapenda sana mbwa ikilinganishwa nap aka.
  • Alisema kwamba hawezi akam’adopt mtoto wa mtu kwa vile hajui kazaliwa na nani, hivyo anasalia tu kuwalea wanyama kama mbwa.



MUIGIZAJI wa muda mrefu wa filamu za Bongo, Wema Sepetu ametoa kauli ya kujisikitikia akisema kwamba hamu yake ya kuitwa mama imeshatoweka kabisa.


Akizungumza na waandishi wa Habari katika hafla ya kisiasa ya chama cha CCM nchini kwao, mrembo huyo ambaye kwa miaka kadhaa amekuwa akionyesha hamu yake ya kuitwa mama alisema kwamba hana Imani tena kama atapata mtoto wa kwake.


Wema alisema kwamba kwa umri aliofikia, yeye atabakia tu ku’adopt mbwa na kuwalea, akisema kwamba yeye anapenda sana mbwa ikilinganishwa nap aka.


Alisema kwamba hawezi akam’adopt mtoto wa mtu kwa vile hajui kazaliwa na nani, hivyo anasalia tu kuwalea wanyama kama mbwa.


“Mimi kuwa na mbwa sioni kama ni kitu cha ajabu sana, mimi ni mpenzi wa mbwa. Sipendi paka kabisa na siwezi kuacha kupenda mbwa eti kwa sababu watu wanasema napenda mbwa.”


“Mbwa wangu Manunu namchukulia kama mtoto wangu, kwa kweli sijafanikiwa kupata mtoto na kiukweli kwa wakati huu hata mkinifariji kwa maneno ya kunitakia kila la kheri katika kutafuta mtoto, mimi nimeshafika umri wa miaka 35 sasa na sitegemei kwamba nitashika mimba tena.”


“Kwa umri wangu sasa miaka 35, safari yangu ya kutafuta mtoto pia imefika mwisho. Hata ile hamu haipo, umefika wakati nimekata tamaa,” Sepetu alisema kwa kujisikitikia.


Alidokeza kwamba ameamua kuishi na ukweli kwamba hatowai mpakata mwanawe katika mikono yake kwa vile ameshaambiwa ana matatizo na huo ndio ukweli alioukubali.


“Na hata ikisemwa kwamba ikitokea sasa hivi… kwanza sidhani kama itatokea kwa sababu tayari yaani nilishaamua kama nimeshaambiwa bwana wewe una matatizo basi ishi nayo, na ndio hivyo mwenyezi Mungu ndio kaamua,” aliongeza.


Alipoulizwa ikiwa ataolewa na mume wake atake mtoto, Sepetu alisema kwamba ikitokea basi mume wake sharti awe mtu wa kuelewa kwamba yeye ana shida.


“Kama atakuwa anajua shida zangu basi itabidi aishi nazo kwa sababu huwezi ukampenda mtu halafu hukubali shida zake. Ukimpenda mtu mchukue na matatizo yake na mapungufu yake na kila kitu chake.”


“Mimi nimeshakubali, nimesema Alhamdulillah kwa sababu nimemtaka [mtoto] kwa muda mrefu, lakini mwenyezi Mungu akaona kwamba labda sistahili na huwezi kumpinga Mungu,” Sepetu aliongeza.


Hata hivyo, mrembo huyo alisema kwamba kutopata kwake mtoto kutamfanya kuwachukia watoto.


“Nitawapenda watoto wa ndugu na marafiki zangu, huwezi jua kwa nini Mungu kaamua kuninyima mimi. Ninashukuru Mungu japo inaniuma sana lakini ndio hivyo tena, maisha yanaenda,’ alimeza mate machungu.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved