logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Baada Ya Kuzama Kimaisha, L-Jay Maasai Akutana Na Yesu Tena Na Kuinuka Upya!

Msanii huyo alifafanua msukumo wake wa kuandikwa wimbo wa Ashomi Shomo akisema kwamba ni kuzingatia simulizi ya kweli ya maisha ambayo ameyapitia katika miaka ya hivi karibuni.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani27 January 2025 - 13:17

Muhtasari


  • Miaka 3 baadae, Maasai ameibuka kijasiri na kuandikwa tungo hiyo ya Ashomi Shomo akisimulia kukutana na Yesu na kuanza ukurasa upya wa maisha.
  • Bila shaka, hii ni hatua ya kijasiri ambayo si wengi wanaimudu kujikung’uta mavumbi na kuanza tena!



MSANII aliyejizolea umaarufu miaka ya 2010s kutokana na nyimbo zake za injili haswa kwa lugha ya Kimaasai, L-Jay Maasai amerudi upya katika tasnia ya injili.


Maasai ambaye amekuwa akipitia changamoto nyingi za maisha tangu mwaka 2022 alikwenda kimya lakini amefanya ujio wa kishindo katika injili ya Kimaasai na wimbo wake mpya ‘Ashomi Shomo’ – tafsiri yake kukutana na Yesu.


Akisimulia ujio wake baada ya muda mrefu wa changamoto za kimaisha zilizomsababishia msongo wa mawazo mwaka 2022, L-Jay Maasai amefichua kwamba amezaliwa upya na kuanza maisha mapya  katika kanisa la Enlightened Christ Embassy – ECE.


“Ninapoanza safari mpya na kutembea na Kristo , Huyu ndiye "MWANA WA UDONGO" aliyezaliwa mara ya pili, aliyerejeshwa na kurekebishwa katika Kanisa la Enlightened Christ Embassy Church (ECE). Chini ya uangalizi mzuri na mwongozo wa Baba yangu Nabii, Brian Omondi,” Maasai alisema.


Msanii huyo alifafanua msukumo wake wa kuandikwa wimbo wa Ashomi Shomo akisema kwamba ni kuzingatia simulizi ya kweli ya maisha ambayo ameyapitia katika miaka ya hivi karibuni alipozama kwenye msongo wa mawazo.


“Imekuwa safari, iliyojaa taabu na mitego, haikuwa rahisi kushinda changamoto na kupigana kupitia vita lakini leo, ninasimama kama shahidi na ninaweza kushuhudia kwa fahari rehema, kibali na baraka za Mungu. Hakika Yeye ni mwaminifu.”


“Kuhusiana na hili Nawaleteeni "Ashomi Shomi" wimbo unazungumzia vita yangu ya muda mrefu ya mambo ya kidunia" yaliyojaa Unyogovu na kushindwa licha ya kuwa LJay Maasai. Ni utambuzi kwamba tunaweza tu kuamini na kukaa chini ya mbawa za Mungu, haijalishi. kile ambacho maisha yanatupa kwa sababu Yeye ni Mwaminifu, mwadilifu na Mungu wa nafasi ya Pili Yeremia:29;,” alifafanua.



Masaibu ya L-Jay Maasai yalifahamika wazi kwenye jamii ya mitandao ya kijamii Februari 2022 alipojitosa kwenye Facebook na kuandikwa barua ndefu akisimulia alivyokuwa anateseka na kuumia maishani licha ya kujijengea jina la kibabe kwenye sanaa ya muziki wa injili.


Katika barua hiyo ya kumlalamikia mkewe, Msanii huyo alisimulia kwa uchungu jinsi familia yake ilisambaratika baada ya mkewe kumuacha na kumzamisha zaidi kwenye lindi la mawazo yasiyojua kupoa.


“Ninaamini unajua mpenzi wangu kwamba nimeumia sana na nimesumbuliwa mno na msongo wa mawazo, wasiwasi, mafadhaiko na unyongovu, mpaka nimefikiwa kiwango ninakosa ladha hata katika Maisha yenyewe. Muda mwingine nimefika mahali mpaka nafikiria kujiuwa. Kwa kifupi, ninahisi nimepoteza maana katika dunia hii,” sehemu ya ujumbe huo mrefu ilisoma.

Maasai pia alizidi kujieleza katika barua hiyo na kumwambia aliyekuwa mkewe Flo Mutia ni kwa jinsi gani amembeza katika Maisha yake kwamba katika kila jambo amekuwa akifanya, mkewe yuko katika mawazo yake hata kama hakuwa anamuona kwa macho.

“Ni mengi ambayo naweza kuandika lakini siwezi hitimisha barua hii bila kukuambia ni kwa jinsi gani nimekuwa nikiumia bila uwepo wako maishani mwangu. Siku zote utabakia kuwa namba moja kwangu, haijalishi mahali nitaenda, chenye nitafanya au chenye nitasema,” alifikia kikomo L-Jay Maasai.


Miaka 3 baadae, Maasai ameibuka kijasiri na kuandikwa tungo hiyo ya Ashomi Shomo akisimulia kukutana na Yesu na kuanza ukurasa upya wa maisha.


Bila shaka, hii ni hatua ya kijasiri ambayo si wengi wanaimudu kujikung’uta mavumbi na kuanza tena!



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved