logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Umechoka Kuni’gift Ama Umesota?” Diana Marua Amkabili Bahati Kwa Nini Aliacha Kumzawidi

“Haujanipa surprise nyingine yoyote. Zawadi ya mwisho ambayo ilinipa ni Range Rover. Hujanizawidi tena, hujashughulika tena na mimi…na unajua mimi ni Mjaluo…” Diana alilalamika.

image
na MOSES SAGWE

Burudani29 January 2025 - 14:35

Muhtasari


  • Bahati kwa kujitetea, alisema kwamba uchumi wa Kenya hauko vizuri vile na kwamba hakuna mtu ambaye Januari hii ako na pesa.
  • ‘Hakuna mtu ambaye hajasota sasa hivi, na huu uchumi kuna mtu hajasota kweli?’ Bahati alisema akimjibu mkewe.



YOUTUBER Diana Marua amezua minong’ono kwenye mitandao ya kijamii baada ya kuonekana kwenye video akimkabili mumewe Bahati Kioko kuhusu ni kwa nini aliacha kumdekeza kwa zawadi.


Wapenzi hao walikuwa wametembelea moja ya mashamba walioyonunua mwaka jana huko Ngong wakati Diana alimhoji Bahati kwa nini hataki kumwekea mradi katika shamba hilo ili kumuingizia faida.


Diana alisema kwamba Bahati amekuwa bahili katika siku za hivi karibuni kiasi kwamba hata hakumbuki ni lini mara ya mwisho alimpa zawadi.


Alimkabili akitaka kujua nini kilibadilika akaacha kumdekeza kwa zawadi, na kuhoji iwapo mumewe alifilisika.


“Mimi nataka mali kila mahali, wewe hakikisha tu ninapata mali ndio mwisho wa siku ninatengeneza faida kutokana na hiyo mali. Sikiliza, umechoka kunitunuku zawadi? Umesota?” Diana alimkabili Bahati.


Bahati kwa kujitetea, alisema kwamba uchumi wa Kenya hauko vizuri vile na kwamba hakuna mtu ambaye Januari hii ako na pesa.


‘Hakuna mtu ambaye hajasota sasa hivi, na huu uchumi kuna mtu hajasota kweli?’ Bahati alisema akimjibu mkewe.


“Hivyo tuseme hutaki kuni’surprise? Kusema tu ukweli ni lini mara ya mwisho ilini’surprise? Ni lini mara ya mwisho ulisimamisha Kenya kwa kunizawidi?” Diana alimuuliza tena.


Mama huyo wa watoto 3 alisema kwamba zawadi ya mwisho alipokea kutoka kwa mumewe ni gari aina ya Range Rover.


 “Haujanipa surprise nyingine yoyote. Zawadi ya mwisho ambayo ilinipa ni Range Rover. Hujanizawidi tena, hujashughulika tena na mimi…na unajua mimi ni Mjaluo…” Diana alilalamika.


Kwa mujibu wa Diana, angetegemea Bahati angempa bonge la surprise kama kumweka kwenye mabango makubwa ya barabarani nchini kote.

Alisema kwamba Bahati sawa tu na wanaume wengine, zawadi ghali na ya maana ambayo

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved