logo

NOW ON AIR

Listen in Live

‘Huna Shukrani Hata Baada Ya Kuchangiwa Sh8.4m’ – Baba T Amlipua Nyanyake Chira

Kwa mujibu wa Baba Talisha, bibi huyo anafaa kuwa mwingi wa fadhila kwa jamii ya TikTokers waliochanga zaidi ya Sh8m kumjengea nyumba ambayo sasa anataka kuuza.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani12 February 2025 - 14:04

Muhtasari


  • Nyumba inayozungumziwa inayojulikana kwa upendo kama "Chira Clan," ilijengwa kama kumbukumbu kwa mtayarishaji maudhui marehemu Brian Chira.
  • Kabla ya kifo chake cha kusikitisha, Chira alikuwa na ndoto ya kuandaa nyumba nzuri kwa nyanya yake.
  • Kwa heshima ya ndoto yake, jamii ya TikTok ilikusanyika pamoja, na kuchangisha Ksh8.4m ili kumjengea nyumba iliyo na samani kamili. 

Faustine BABA Talisha na nyanyake Brian Chira

TIKTOKER Baba Talisha amemshambulia vikali nyanyake aliyekuwa TikToker Brian Chira kwa kile anadai kwamba bibi huyo hana shukrani.


Kupitia chapisho lenye aya ndefu kwenye ukurasa wake wa Instagram, Fastine Lipuku Lukaale, maarufu kama Baba T alimzomea nyanyake Brian Chira kwa kuendelea kuwataka TikTokers kumsaidia zaidi.


Kwa mujibu wa Baba Talisha, bibi huyo anafaa kuwa mwingi wa fadhila kwa jamii ya TikTokers waliochanga zaidi ya Sh8m kumjengea nyumba ambayo sasa anataka kuuza.


Baba Talisha alisema kwamba bibi huyo anafaa kuwa na shukrani kwani hakuna mtu mwingine nchini amewahi changiwa kiasi hicho cha fedha, lakini kwa mshangao wa wengi, anataka kusaidiwa zaidi.


"Ninahisi aibu kuona mtu ambaye amesaidiwa na familia ya mtandaoni, haswa kwenye TikTok, akiwa hana shukrani. Ksh8.4 milioni zilikusanywa. Ilisalia na Ksh7.4 milioni chini ya mwaka mmoja kwenda chini, hakuna chochote. Hakuna mtu katika historia ya uchangishaji ambaye amesaidiwa kama yeye. Ilikuwa haitoshi kwake,” Baba Talisha alieleza.


Nyumba inayozungumziwa inayojulikana kwa upendo kama "Chira Clan," ilijengwa kama kumbukumbu kwa mtayarishaji maudhui marehemu Brian Chira.


Kabla ya kifo chake cha kusikitisha, Chira alikuwa na ndoto ya kuandaa nyumba nzuri kwa nyanya yake.


Kwa heshima ya ndoto yake, jamii ya TikTok ilikusanyika pamoja, na kuchangisha Ksh8.4m ili kumjengea nyumba iliyo na samani kamili.


Mwaka mmoja baadae, nyanyake Chira ameibuka na madai kwamba eneo iliko nyumba hiyo hakuna usalama wa kutosha na kuonyesha nia ya kutaka kuiuza.


Bibi huyo alitoa wito kwa TikTokers kukaa chini ili kumfikiria tena katika suala la usalama wake la sivyo atalipiga mnada jumba hilo na kuhama.


“Sitauza vitu vyenu bila ruhusa yenu. Nataka mkae chini muone shosho atakaa aje. Kama mtanijengea ua la umeme ama kununua shamba na kunijengea mahali pengine. Kulikuwa na wezi hivi majuzi na nilimpigia Obidan simu lakini hakupokea. Wanaiba ng’ombe na vitu vingine. Hakuna usalama,” nyanyake Chira aliomba.


Suala hilo limeonekana kuwakera baadhi ya TikTokers, Baba Talisha ambaye alikuwa mstari wa mbele kuchangisha fedha hizo akiwa wa hivi punde kuvunja kimya chake.


 



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved