logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Grand P Apata Size Yake Baada Ya Kusuasua Na ‘Gari Kubwa’ Kwa Miaka Mingi

“Bibi Kaba acha yaliyopita yapite Wewe ndiye chanzo cha furaha yangu, na sitamani chochote zaidi ya kuwa nawe kando yangu maishani.”

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani17 February 2025 - 10:38

Muhtasari


  • Kijana huyo amekuwa katika miaka ya nyuma kwenye uhusiano na sosholaiti wa Ivory Coast Eudoxie Yao ambaye ana umbile kubwa maradufu kumliko Grand P.

Grand P na mpenzi wake

MWIMBAJI tajiri wa Guinea Moussa Sandiana Kaba almaarufu Grand P amemtambulisha mpenzi wake mpya, miaka kadhaa baada ya mahusiano yake baridi na sosholaiti kutoka Cote D’Ivoire, Eudoxie Yao.

Kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii, Grand P alichapisha msururu wa picha kadhaa za kimahaba siku ya Ijumaa wakisherehekea siku ya wapendanao.

Msanii huyo mwenye umbo dogo kimwili alimtambulisha Mrembo huyo ambaye ana mwili mdogo kama yeye ambaye alimtambulisha kama ‘Mrs Kaba Mariame’ akirejelea jina lake la ukoo.

“Mabawa ya kuku wangu 🥰 tazama jinsi anavyopendeza 🥰 asante Bwana 🙏 mbaya sana kwa jirani. Bibi Kaba acha yaliyopita yapite 🙏 Wewe ndiye chanzo cha furaha yangu, na sitamani chochote zaidi ya kuwa nawe kando yangu maishani. Njoo karibu na ufariji moyo huu ambao unauliza tu kutetemeka kwa mdundo wa upendo wako,” Grand P alimbemenda kwa huba.

Kijana huyo amekuwa katika miaka ya nyuma kwenye uhusiano na sosholaiti wa Ivory Coast Eudoxie Yao ambaye ana umbile kubwa maradufu kumliko Grand P.

Uhusiano wake na Yao ulionekana kutumbukia mchangani mapema 2023 ambapio kufikia Aprili, alitangaza kuingia katika penzi la mwanadada mwingine aliyeitwa kwa jina Yubai Zhang.

Grand P alitangaza mahusiano yao kupitia akaunti yake ya Facebook akithibitisha mapenzi yake na mrembo huyo wa Kiasia na kuweka wazi kuwa hakuna nafasi ya watu wenye wivu maishani mwao.

"Yubai Zhang wangu, hakuna nafasi kwa watu wenye wivu," alisema chini ya picha zake na Zhang alizochapisha Facebook.

Balozi huyo wa Guinea nchini Mali alikatisha mahusiano yake na mwanamitindo Yao mwaka wa 2021 baada ya kuwa kwenye mahusiano na mwanamitindo huyo kwa takriban miaka mitatu.

Wawili hao walitangaza kukuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi mwaka wa 2020 baada ya kuchapisha picha wakiwa pamoja.

Mahusiano hayo yaliibua gumzo mitandaoni kwa ajili ya uzani wao, mashabiki walishangaa ni vipi Grand P mweye mwili mdogo anaweza kuwa kwenye mahusiano na mwanamke huyo aliyeonekana kumzidi  kwa uzani kwa kiasi kikubwa.

Hata hivyo, haikupita muda mrefu kabla ya kurudiana na Yao tena katika penzi ambalo lilisuasua kwa muda mrefu hadi kukamilika mwaka jana tena.

 

 

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved