logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Metro Trans kuhamasisha wafanyikazi wao Jumamosi kuzuia yaliyowakuta Super Metro

Metro Trans inachukua hatua ya kutoa mafunzo upya kwa madereva na makondakta wake ili kuzuia hali sawa na ile iliyowakuta wenzao wa Super Metro waliopigwa marufuku na NTSA

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani20 March 2025 - 16:24

Muhtasari


  • Hafla hiyo ya kutoa mafunzo kwa madereva na makondakta wao itafanyika Jumamosi, Machi 22, hivyo hawatakuwa barabarani kutoa huduma za usafiri na watarejea barabarani Jumapili na Machi 23. 

Metro Trans

KAMPUNI ya magari ya uchukuzi wa umma jijini Nairobi na Maeneo jirani, Metro Trans imetangaza kuandaa warsha ya kutoa mafunzo na hamasisho kwa madereva, makondakta na wafanyikazi wao wengine.

Kupitia machapisho kwenye kurasa zao za mitandao ya kijamii, Metro Trans walitangaza kwamba hafla hiyo ya kutoa mafunzo kwa madereva na makondakta wao itafanyika Jumamosi, Machi 22, hivyo hawatakuwa barabarani kutoa huduma za usafiri.

Metro Trans ilisema itarejea barabarani Jumapili na Machi 23 kuendelea na hukuma kwa watumizi wa usafiri wa umma.

“Ili kuendelea kukuhudumia vyema zaidi, tumepanga programu ya uhamasishaji kwa madereva, makondakta na wafanyakazi wetu siku ya Jumamosi, tarehe 22 Machi 2025. Kwa sababu hiyo, huduma zetu zote zitasitishwa siku hii. Tutarejelea shughuli za kawaida Jumapili, tarehe 23 Machi 2025. Tunaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaosababisha na tunathamini usaidizi wako unaoendelea,” taarifa ilisema. 

Metro Trans inachukua hatua ya kutoa mafunzo upya kwa madereva na makondakta wake ili kuzuia hali sawa na ile iliyowakuta wenzao wa Super Metro waliopigwa marufuku kuhudumu barabarani na mamlaka ya NTSA.

Mapema Alhamisi, NTSA ilitaarifu umma kwamba sacco ya Super Metro imepigwa marufuku kuhudumu barabarani katika kile walisema kwamba magari mengi ya sacco hiyo yamekiuka masharti ya kuhudumu.

NTSA ilitahadharisha umma dhidi ya kuabiri magari ya sacco hiyo na kutoa angalizo kwa maafisa wa Trafiki kuyazuia magari ya sacco hiyo yatakayokiuka marufuku hiyo.

“Hii ni kuufahamisha Umma kwamba Mamlaka imesimamisha leseni ya waendeshaji wa Super Metro Limited hadi Kampuni itii kikamilifu Kanuni za Magari ya Utumishi wa Umma, 2014 na masharti mengine yaliyowekwa,” sehemu ya chapisho hilo ilisema.

 “Wananchi wametahadharishwa dhidi ya kupanda gari la kampuni ya Super Metro Limited. Idara ya Trafiki inahitajika kukamata magari ya Kampuni ambayo yatapatikana yakifanya kazi kinyume na kusimamishwa,” tangazo hilo lilisomeka zaidi.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved