logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ndoto yangu ilikuwa kuwa mwalimu au mwanajeshi - Karen Simba

Simba sasa anaeleza kwamba tangu zamani alikuwa na ndoto ya kuja kuwa mwalimu au mwanajeshi.

image
na Japheth Nyongesa

Burudani24 March 2025 - 09:30

Muhtasari


  • Mwanadada Simba ni mmoja kati ya waigizaji wa kitanzania ambao ndoto yao iling'aa kwa wakati mmoja.
  • Muigizaji huyo kwa sasa ana umri wa miaka 23.
Caren Simba
Mwanamitindo maarufu kutoka nchini Tanzania Karen Simba ambaye jina lake halisi ni Esther Simba sasa anaeleza kwamba tangu zamani alikuwa na ndoto ya kuja kuwa mwalimu au mwanajeshi.

Simba alikuwa anazungumza haya kwenye mahojiano na mwanahabari. Alieza kwamba alikuwa anavutiwa sana na kuwa mwanajeshi baada ya kuwa mwanaskauti kwa siku nyingi na kujifunza mengi.

Wakati akizungumza pia ameweka wazi kwamba wakati alitaka kuwa mwanajeshi hakuwa na tamaa ya kuolewa au kupata mtoto.

"Kipindi niko shule, cha kwanza nilikuwa natamani nije kuwa mwalimu. Baadaye nikaja nikabadilisha mawazo nikasema natakia kuwa mwanajeshi. Nilikuwa na ndoto mbili, kati ya hizo mbili mwenyewe nilikuwa natamani sana kuwa Jeshi," aliweka wazi Mwanamitindo Simba.

"Tulikuwa tunafanya sikauti na nikapewa uwenyekiti na kuna vitu nilikuwa najifunza huko na nikatamni siku moja nije kuwa kamanda. Kidogo ilifika mahali nikaona ni vigumu kuingia jeshi," alieleza.

Akizungumza alifichua kwamba hakuwa na tamaa ya kuolewa wakati akiwa na ndoto ya kuwa mwanajeshi. "Kwa kipindi kile sikuwa na mwawazo ya kuolewa au mawazo ya kuzaa,"

Mwanadada Simba ni mmoja kati ya waigizaji wa kitanzania ambao ndoto yao iling'aa kwa wakati mmoja baada ya kuachilia video ya 'Siri ya Moyo'

Muigizaji huyo kwa sasa ana umri wa miaka 23, ashawahi kuleza kwamba maisha yake ya zamani hayakuwa mazuri hasa baada ya kushindwa kukamilisha masomo yake kutokana na changamoto za karo ya shule.





RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved