logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Diamond achoshwa na kutumia Rolls Royce, aangazia macho yake kwa Bugatti

“Nimechoka na hii Rolls Royce, siwezi ngoja Bugatti langu kuwasili nyumbani,” Diamond aliandika.

image
na MOSES SAGWE

Burudani07 April 2025 - 10:27

Muhtasari


  • “Nimechoka na hii Rolls Royce, siwezi ngoja Bugatti langu kuwasili nyumbani,” Diamond aliandika.
  • Diamond alionyesha gari hilo kwa mara ya kwanza mwishoni mwa 2020 likiwa na nambari binafsi ya usajili yenye jina lake, Platnumz.

Diamond Platnumz na gari lake la kifahari, Rolls Royce//INSTAGRAM

MSANII maarufu wa miziki ya Bongo Fleva, Diamond Platnumz amedokeza kuchoshwa na gari lake la kifahari – Rolls Royce.

Kupitia Instagram stories zake, Diamond alichapisha picha ya gari hilo la kifahari lenye rangi ya samawati na kufuatisha na ujumbe kwamba amechoka kulitumia na sasa anajiandaa kupokea gari jingine la kifahari aina ya Bugatti.

Alidokeza kwamba Bugatti limo njiani linasafirishwa kutoka ughaibuni na pindi litakapofika, utakuwa mwisho wake wa kutumia Rolls Royce ambalo alinunua takribani miaka 5 iliyopita.

“Nimechoka na hii Rolls Royce, siwezi ngoja Bugatti langu kuwasili nyumbani,” Diamond aliandika.

Diamond alionyesha gari hilo kwa mara ya kwanza mwishoni mwa 2020 likiwa na nambari binafsi ya usajili yenye jina lake, Platnumz.

Baadae Julai 2021, alibadilisha nambari hiyo ya usajili na kuweka ‘SIMBA’ katika kile kilichoonekana kama ni kutimiza ndoto zake za muda mrefu.

Itakumbukwa Wakati fulani mwaka wa 2018 alisema katika mahojino kwamba angelinunua gari hilo ‘hivi karibuni’

Baada ya kulinunua, Diamond aliamsha popo kwenye Instagram baada ya kuweka kwenye bio yake kwamba ndiye mwanamuziki wa kwanza kutoka Afrika Mashariki kumiliki gari la Rolls Royce.

Mwaka wa 2016 nyota huo alionekana katika gari la   jeupe la  Rolls Royce  lakini baadaye ikagunduliw akwamba alikuwa akifanya video ya wimbo wake

Gari kama hilo lenye gharama ya juu ni  Rolls-Royce Phantom  lilimgharimu kati ya $450,000 ( takriban  shilingi  45,000,000) kipindi hicho.

Diamond anafahamika kwama mpenzi wa magari na wakati mwingi huyataja kama  ‘my babies’

 

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved