logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Masauti akiri kumnyima meneja wake chupi aliyorushiwa jukwaani na shabiki wa kike

Masauti hata hivyo alisema kwamba baadae alikutana na mwenye kumrushia chupa na ‘kumalizana naye’.

image
na MOSES SAGWE

Burudani16 April 2025 - 09:32

Muhtasari


  • “Halafu meneja si unajua lazima amlinde msanii, hivyo aliniambia leta hapa, nikamwambia baba eh, hii nimetupiwa mimi, sasa wewe unataka nikupe kwa mpango gani?"
  • "Nikamwambia tulia wacha nicheze nayo hii mpaka nimjue mwenye chupi ni nani,” Masauti alielezea tukio zima.

Masauti//Instagram

MSANII Masauti kutokea Pwani ya Kenya kwa mara nyingine amezungumzia kisa kilichomsibu Mtwapa mwaka jana wakati akitumbuizia mashabiki wake.


Akizungumza katika mahojiano kwenye kituo kimoa cha redio humu nchini siku chache zilizopita, msanii huyo alirejelea kisa hicho ambapo alitupiwa nguo ya ndani na shabiki mwanamke wakati anatumbuiza kwenye jukwaa.


Masauti alikiri kwamba lilikuwa ni tukio la kustaajabisha na la kumpunga vile vile kwani hakuwahi fikiria angefanyiwa kitendo hicho na shabiki wa kike, akiitaja kama ishara ya mashabiki kumkubali kimuziki.


Katika kisa hicho kilichotokea mwaka jana, Masauti Alifichua kwamba baada ya kuidaka ile chupi, meneja wake alitaka akabidhiwe lakini Masauti akakwama nayo kabla ya kuinusa.


“Mwanzo Ilikuwa ni vibe nilikuwa niko shoo pale yatch watoto wa kike wakapagawa kumuona Masauti. Mtoto Fulani ambaye mimi sielewi anatokea wapi nashangaa ananirushia jichupi la pink. Nililidaka mwanzo nikashangaa duh!”


“Halafu meneja si unajua lazima amlinde msanii, hivyo aliniambia leta hapa, nikamwambia baba eh, hii nimetupiwa mimi, sasa wewe unataka nikupe kwa mpango gani? Nikamwambia tulia wacha nicheze nayo hii mpaka nimjue mwenye chupi ni nani,” Masauti alielezea tukio zima.


Masauti hata hivyo alisema kwamba baadae alikutana na mwenye kumrushia chupa na ‘kumalizana naye’.


“Chupi nilimrejeshea mwenyewe. Mwenye chupi tulimalizana,” Masauti alidakia.


Masauti akizungumzia tukio kwa mara ya kwanza mwaka jana, alisema kwamba hakuwa anatarajia hilo kwani kwa muda mrefu alikuwa anajua matukio hayo wanafanyiwa wasanii wa nchi za Magharibi na Ulaya.


“Nilirushiwa chupi, sijawahi kurushiwa chupi kwenye steji ila kwa mara ya kwanza nilirushiwa. Kwa yule ambaye alirusha bigup sana kwa sababu alinifanya nikajihisi vizuri, unajua video za kurushiwa chupi tushaziona kwa wasanii kina Drake sijui kina Burna Boy, halafu sasa mimi hapa Masauti pia nimekuwa msanii wa kwanza Mombasa kurushiwa chupi,” alisema.


 


Makala Zinazohusiana

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved