logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Sandra Dacha arejesha udhibiti wa akaunti yake ya Facebook, miezi 14 baada ya kudukuliwa

Akaunti hiyo ilidukuliwa ikiwa na wafuasi 962,000 mnamo Februari 2024 na kumuacha Dacha akiwa anategemea akaunti ya Kibinafsi kwenye ukurasa huo.

image
na MOSES SAGWE

Burudani16 April 2025 - 13:44

Muhtasari


  • Kupitia kwa akaunti mbadala, Dacha alitangaza kupata udhibiti kamili wa akaunti hiyo ambayo imekuwa mikononi mwa wadukuzi kwa zaidi ya mwaka mmoja.
  • Akaunti hiyo ilidukuliwa ikiwa na wafuasi 962,000 mnamo Februari 2024 na kumuacha Dacha akiwa anategemea akaunti ya Kibinafsi kwenye ukurasa huo.

Sandra Dacha

MUIGIZAJI Sandra Dacha hatimaye amepata furaha baada ya akaunti yake ya Facebook yenye wafuasi takribani milioni moja kurejeshwa chini ya udhibiti wake.

Kupitia kwa akaunti mbadala, Dacha alitangaza kupata udhibiti kamili wa akaunti hiyo ambayo imekuwa mikononi mwa wadukuzi kwa zaidi ya mwaka mmoja.

Dacha alikumbuka siku ambayo hiyo akaunti ilipodukuliwa mnamo Februari mwaka jana, alishindwa kulala na hata hamu yake ya kula ilipotea akabaki akilia bila msaada.

“Februari mwaka jana, ukurasa wangu wa Facebook ulidukuliwa. Na acheni niwaambie, maisha yangu hayajawahi kuwa sawa tena. Siku ambayo ilidukuliwa, nilishindwa kula, nilishindwa kulala, nililia, nikawika na kulia tena,” Sandra Dacha alisema.

Alishukuru usimamizi wa Facebook na rafiki yake Martin Githinji kwa kuwa wa msaada mkubwa kwake ambapo amekuwa akifuatilia mchakato wa kurejeshwa kwa akaunti hiyo mikononi mwake.

Alimtania Githinji kwamba kama si hali ya uchumi wa sasa, angempa zawadi ya Ndege aina ya helikopta.

“Lakini acheni niwaambie, baada ya panda-shuka zote, ninafuraha kutangaza kwamba akaunti hii imerudi kwangu, hallelujah. Shukrani zote ziende kwa Martin Githinji na timu ya Facebook.”

“Wewe Marto wewe aki ya Mungu kama sio huu uchumi ningekununulia chopper. Pole kwa kukusumbua katika muda wote huu,” Dacha aliongeza.

Akaunti hiyo ilidukuliwa ikiwa na wafuasi 962,000 mnamo Februari 2024 na kumuacha Dacha akiwa anategemea akaunti ya Kibinafsi kwenye ukurasa huo.

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved