logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Lukamba amtaka Diamond kuwalipa wafanyikazi vizuri, aitaja Wasafi kama jehanamu

“Unajitahidi kuaminisha watu uongo. Kama kuna mtu kavunja rekodi yangu ajitokeze. Nina mwaka wa pili tangu nitoke jehanamu. Bwana wee hakuna maisha hapo, ni njaa kali sana.”

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani17 April 2025 - 12:35

Muhtasari


  • Alidai kwamba Wasafi ndio huwafanya watu kuwa mstaa lakini akasema kwamba mwisho wa siku watu hawali na kuishi ustaa na kumtaka Diamond kuboresha mishahara yao.
  • “Walipeni watu vizuri, watu wanajitoa sana wanafanya kazi nzuri ambazo mpaka leo mnajivunia kazi zao. Nani atakula ustaa bila hela?” Lukamba alihoji.

Diamond na aliyekuwa mpiga picha wake Lukamba//MAKTABA

ALIYEKUWA mpiga picha wa Diamond Platnumz, Lukamba ameibuka kwa mara nyingine, safari hii akielekeza mtutu wake wa mashambulizi kwa bosi wake wa zamani.

Kupitia msururu wa maneno makali kwenye insta stories zake, Lukamba alidai kwamba wafanyikazi wa Wasafi wote wanalipwa mishahara duni licha ya kufanya kazi kubwa.

Alisema kwamba miaka 2 tangu aondoke Wasafi, hakuna mfanyikazi ambaye amevunja rekodi ya kufanya kazi jinsi yeye alikuwa akifanya, lakini malipo yake ni ya kijungu jiko.

Msanii huyo aliitaja Wasafi kama jehanamu, akimtaka bosi wao Diamond kuwafanyia haki ya mishahara mizuri watu wanaojimaliza kulitetea jina lake kama kina Baba Levo.

“Unajitahidi kuaminisha watu uongo. Kama kuna mtu kavunja rekodi yangu ajitokeze. Nina mwaka wa pili tangu nitoke jehanamu. Bwana wee hakuna maisha hapo, ni njaa kali sana.”

“Diamond! Diamond nani wewe, kawa Mungu? Acheni kudanganya watu sasa, nitayamwaga,” Lukamba alitishia.

Alidai kwamba Wasafi ndio huwafanya watu kuwa mstaa lakini akasema kwamba mwisho wa siku watu hawali na kuishi ustaa na kumtaka Diamond kuboresha mishahara yao.

“Walipeni watu vizuri, watu wanajitoa sana wanafanya kazi nzuri ambazo mpaka leo mnajivunia kazi zao. Nani atakula ustaa bila hela?” Lukamba alihoji.

Alidai kwamba Wasafi imekimbiwa na wafanyikazi wengi kutokana na uongo, huku pia akidai kwamba baadhi ya wacheza densi ambao waliondoka na kwenda Marekani wamefanya maendeleo makubwa chini ya mwaka tangu kugura kibarua cha Diamond.

“Imagine madensa wameng’ang’ana miaka 10 bila chochote maskini mpaka wamekimbia zao Marekani mwaka mmoja wameshajenga. Wangekufa njaa,” aliongeza.

Lukamba pia alikariri kwamba ufichuzi huo wake si wa kutafuta kiki akisema kwamba watu wa Wasafi kina Baba Levo ndio walioanza kumshambulia.

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved