logo

NOW ON AIR

Listen in Live

PATANISHO: Mke wangu nampenda kama machungwa! - Mburu

PATANISHO: Mke wangu nampenda kama machungwa! - Mburu

image
na

Dakia-udaku02 October 2020 - 04:27
Leo katika kitengo cha Patanisho aliyeomba kupatanishwa ni jamaa kwa jina Julius Mburu, 46,  akidai walikosana na mkewe bi Nancy, 42, miezi misita iliyopita.

"NIlikuwa naishi Nairobi naye ushago na tulikosana baada ya watu kunieleza kuwa alikuwa na mipango ya kando. Nilipomuuliza kuhusu madai hayo akaondoka na kwenda kwao."

Mburu aliongeza akidai kuwa kwa miezi sita sasa kila anapojaribu kuzungumza naye mkewe huwa anadinda.

Nataka tupatanishwe kwani nimepeleka mahari tayari na ni wangu!" Aliongeza.

Wawili hao wamekuwa kwa ndoa ya miaka 23 na kifungua mimba wake ana miaka 22 na mkewe ndiye anaishi na wanao.

Bi Nancy alipopigiwa simu alisema kuwa hawezi zungumza sasa hivi kwani yuko kazini. Isitoshe alisema Mburu akawaombe wazazi wake msamaha ila sio yeye.

"Uliwatusi wazazi wangu kwa hivyo sio mimi anaomba msamaha, isitoshe alitusi watoto na kuwakana." Alisema Nancy kabla ya Mburu kumlaumu shetani.

Isitoshe bi Nancy alisema mumewe amekuwa na mazoea kwani hii ni mara ya tatu.

Aki nampenda mke wangu sijui kama nini....labda machungwa! Mburu alijitetea.
Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved