logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Story Za Ghost: 'Nyoka ilimeza pesa zote!' Mhasibu wa Nigeria ajitetea

Story Za Ghost: 'Nyoka ilimeza pesa zote!' Mhasibu wa Nigeria ajitetea

image
na

Habari02 October 2020 - 05:21
Katika kitengo cha Story za Ghost Mulee, mtangazaji huyu mcheshi aliwaacha wengi wakiangua kicheko baada ya kusimulia kisa kimoja cha kushangaza kilichotokea nchini Nigeria.

Kulingana na Ghost, mhasibu (accountant) mmoja nchini humo aliwashangaza wengi baada ya kupatikana katika sakata ya ufujaji wa pesa.

Mhasibu huyo kwa jina Philomena Chiesa, alijipata matatani baada ya mkaguzi wa kifedha kubagua kuwa kitita cha millioni kumi hakibainiki kiliko katika shirika analofanyia kazi.

Na alipoulizwa fedha hizo ziliko alijitetea akisema kuwa kuna nyoka ambaye alimeza zile fedha zote, huku akiwaacha wengi na butwaa.

Soma usimulizi wake Ghost Mulee,

Wajua nchi ya Kenya na Nigeria kuna vitu kadhaa ambazo zafanana, kwa mfano hapa kuna EACC ya kupigana na ufisadi, Nigeria kuna EFC.

Kuna accountant anayejulikana kama Philomena Chiese na auditors walipofanya hesabu ikabainika kuwa millioni kumi hazijulikano ziliko.

Alipoulizwa mwanadada yule alisema kuwa fedha zile zimeliwa na nyoka.

"Nimeambiwa na mfanyikazi wangu na mfanyikazi mwenza kuwa zile fedha zimeliwa na nyoka, na sijui mnacho zungumzia kwani nyoka ilimeza fedha zote." Alisema yuke mwanadada.

Mwanadada yule kwa sasa amekamatwa na uchunguzi unaendelea.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved