logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Cheche zaibuka baina ya mirengo inayoshabikia upande wa Ruto na Gideon Moi

Cheche zaibuka baina ya mirengo inayoshabikia upande wa Ruto na Gideon Moi

image
na

Dakia-udaku02 October 2020 - 07:42
55ft1JC2.jfif
Ubabe wa uongozi haswa katika jamii ya Kalenjin nchini unatazamiwa kuchukuwa mkondo mwengine baada ya viongozi wanaoshabikia upande wa Ruto na Gedion Moi kuanza kukabiliana kwa maneno makali baada ya Ruto kuzuru wazee wa Talai wiki jana.

Viongozi wanaoegemea upande wa seneta wa Baringo Gedion Moi,wamekashifu hatua ya Ruto kujiwasilisha katika eneo kuombewa na wazee hao wakisema walikuwa wanapania kumuombea Gedion kama kiongozi wao.

Akiwa kwa mazungumzo na jarida moja la humu nchini,katibu mkuu wa chama cha KANU Nick Salat amesema ni wazi kuwa Ruto ni kiongozi ambaye anajitakia makuu bila ya kulijali taifa ama jamii yake ya Kalenjin.

Salat alisema baadhi ya viongozi wa wazee hao walikuwa wanapania kumuombea Moi na kuwa kiongozi wao wa kisiasa.

"He has been blasting others for visiting shrines but what happened is a sign of desperation and wants the community to sympathise with him,"amesema Salat.

Salat ameongezea kuwa hakuna mtu yeyote kutoka Rift Valley anayemuonea huruma Ruto kwa yale anayopitia baada ya kuamua kulemaza utendakazi wa rais Kenyatta.

"The Friday meeting had no impact on us at all,amesema Salat.

Aidha wazee hao wa Talai walisema kuwa hakna njama fiche katika maombi yao kwani walikuwa wanamuombe tu Ruto.

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved