logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wanawake 2 wakamatwa kwa jaribio la udanganyifu Mwea Mashariki

DCI alisema katika taarifa kupitia Twitter kwamba wawili hao walionekana wakitoka kwenye chumba hicho

image
na Radio Jambo

Dakia-udaku12 April 2021 - 14:45

Muhtasari


  • DCI yawakamata wanawake 2 kwa jaribio la udanganyifu mwea mashariki

Wapelelezi wa DCI Jumatatu waliwakamata wanawake wawili kwa madai ya kupumbaza na kujaribu kumwibia mwanamume huko Mwea Mashariki.

Grace Njeri na Evelyne Esendi wenye umri wa miaka 29 na 32 wanashukiwa kuwekea chumba katika nyumba ya wageni ya Village Inn huko Mwea Mashariki Jumapili na kumshawishi mwathiriwa wao Daniel Gathege Maira kwa mtego wao.

DCI alisema katika taarifa kupitia Twitter kwamba wawili hao walionekana wakitoka kwenye chumba hicho na kuenda katika eneo la ATM, ambapo wapelelezi wanaamini shughuli zingine zilifanywa.

"Ni hatua hii ya tuhuma ambayo ilivutia mdhibiti wa CCTV huko Nice Digital City, ambaye mara moja aliwaonya Maafisa wa Polisi walio katika kituo cha Polisi cha Wanguru.," Kurugenzi hiyo ilisema.

Baada ya uchunguzi zaidi, wahusika wa DCI walimkuta mWANAMUME huyo akiwa amelala kitandani akiwa hajitambui.

Alikimbizwa katika Hospitali ya Misheni ya Comrade ambapo sasa anapokea matibabu.

"Kama mwathiriwa anaendelea kupona, washukiwa wawili wanasalia kizuizini kujibu mashtaka ya udanganyifu," DCI alisema.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved