logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Esma Platnumz azungumzia madai ya Aaliyah kuwa na ujauzito wa Diamond

Alisema huwa anamuona Aaliyah mara kwa mara ila bado hajaona dalili zozote za ujauzito kwake.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri24 March 2022 - 04:15

Muhtasari


•Alisema hana ufahamu wowote kuhusu mahusiano yoyote ya  kimapenzi kati ya kakake Diamond Platnumz na mtangazaji Aaliyah Mohamed.

•Aliweka wazi kuwa huwa anamuona Aaliyah mara kwa mara ila bado hajaona dalili zozote za ujauzito kwake.

Diamond Platnumz na Aaliyah Mohamed

Mfanyibiashara Esma Platnumz amesema hana ufahamu wowote kuhusu mahusiano yoyote ya  kimapenzi kati ya kakake Diamond Platnumz na mtangazaji Aaliyah Mohamed.

Akizungumza na waandishi wa habari katika hafla ya kuzindua video za EP ya FOA, Esma alisema hana uhakika kuhusu jinsi wawili hao wanavyohusiana licha wa karibu nao.

"Aaliyah ni jirani wangu kabisa. Huwa tunaonana na saa zingine huwa tunalala pamoja. Mimi kuwa na Aaliyah sio tatizo. Habari za mimba mimi sijui, na sijui kama ana mahusiano na Naseeb, sijui chochote," Esma alisema.

Mama huyo wa watoto wawili aliweka wazi kuwa huwa anamuona Aaliyah mara kwa mara ila bado hajaona dalili zozote za ujauzito kwake. 

"Aaliyah hana mimba. Namuona yuko kawaida. Yeye ni rafiki yangu, tunakaa katika nyumba moja. Sisi ni majirani na sijaona mimba, sijaona kukata breed," Alisema.

Tetesi kwamba mtangazaji huyo ana mahusiano ya kimapenzi na bosi wake katika Wasafi Media, Diamond zimekuwa zikienezwa kwa muda mrefu.

Mwaka jana madai yaliibuka kwamba wawili hao wanatarajia mtoto pamoja.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved