logo

NOW ON AIR

Listen in Live

BBI: Martha Koome akosoa mchakato wa marekebisho ya katiba

Martha Koome akosoa mchakato wa marekebisho ya katiba

image
na

Dakia-udaku31 March 2022 - 07:58

Muhtasari


• Jaji mkuu Martha Koome amebatilisha uamuzi wa mahakama kuu na ile ya rufaa kuhusu uhalali wa BBI.

• Amesema kwamba sheria ya kuwepo kwa mfumo wa kimsingi haina mashiko humu nchini.

Jaji mkuu Martha Koome amekosoa mchakato wa marekebisho ya katiba maarufu BBI akisema kwamba kanuni za kisheria zilikiukwa.

Koome amekuwa wa kwanza kati ya majaji saba ambao wanatarajiwa kutoa uamuzi wao kuhusu sheria ya mfumo wa kimsingi [basic structure]katika mchakato wa kubadilisha vipengele vya katiba.

"Sheria ya mfumo wa kimsingi haiwezi kutumika hapa Kenya, kwa hiyo mabadiliko yoyote yanapaswa kufanywa tu kulingana na katiba," Koome alisema.

Alizilaumu mahakama kuu na ile ya rufaa kwa kutochunguza na kubaini upungufu wa sheria hiyo ya 'basic structure' na kupuuza hali halisi kwamba katiba ya Kenya inaweza kujisimamia.

Alisisitiza kuwa kumekuwa na hatua kadhaa za kujaribu kuifanyia katiba ya 2010  marekebisho bila mafanikio, hali ambayo inadhihirisha uthabiti wake.

Kulingana na Koome, alitaka kuwepo kwa uwezekano na usawa katika kubadilisha au kutobadilisha vipengele katika katiba.

Hata hivyo, alikubaliana na mahakama hizi za upeo wa chini kwamba rais Uhuru Kenyatta hawezi kuasisi mchakato wa kufanya marekebisho kwenye katiba.

Aidha, alisema kwamba Rais Kenyatta kama Mkenya ana kila haki ya kusimamia na kuasisi mchakato wa kubadilisha vipengele kwenye katiba.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved