logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wanaume 2 wenye umri wa makamo wapatikana wakiwa wamekufa kwenye gari lililoibwa Lucky Summer

Gari hilo lilipatikana likiwa limetupwa katika uwanja wazi huko Gatheca.

image
na Radio Jambo

Dakia-udaku27 May 2022 - 10:36

Muhtasari


  • Wanaume 2 wenye umri wa makamo wapatikana wakiwa wamekufa kwenye gari lililoibwa Lucky Summer

Maafisa wa upelelezi wanajaribu kubainisha miili miwili ilipatikana kwenye gari lililoibwa lililopatikana likiwa limetupwa Lucky Summer, Nairobi.

Gari hilo lilipatikana likiwa limetupwa katika uwanja wazi huko Gatheca.

Mmiliki wa gari nyeupe aina ya Toyota Vitz (KCH 715Z) alikuwa akifuatilia suala la wizi wa gari katika Kituo cha Polisi cha Lucky Summer siku ya Alhamisi.

Polisi kupitia taarifa walisema mmiliki wa gari kisha alipokea simu kutoka kwa rafiki yake kwamba alikuwa ameona gari kama hilo uwanjani.

"Alikwenda eneo la tukio akiwa ameandamana na maafisa wa polisi na alipofika, alitambua gari hilo kuwa lake ingawa nambari za mbele na za nyuma zilikuwa zimetolewa," polisi walisema.

Walipochungulia madirishani, polisi waligundua wanaume wawili wa makamo ndani wakiwa na harufu mbaya iliyokuwa ikitoka kwenye gari.

Miili hiyo ilipelekwa katika chumba cha kuhifadhi maiti cha City ikisubiri kutambuliwa na uchunguzi wa maiti ili kubaini chanzo cha kifo hicho.

 

 

 

 

 

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved