logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mashindano ya watoto ya kuua paka New Zealand yaahirishwa

Tukio hilo lilileta shutuma kutoka kwa vikundi vya ustawi wa wanyama.

image
na Radio Jambo

Dakia-udaku20 April 2023 - 03:42

Muhtasari


•Waandaaji wa msako wa kila mwaka walikosolewa baada ya kutangaza kitengo kipya cha watoto kuwinda paka mwitu nchini New Zealand.

Mashindano ya watoto ya kuwinda paka nchini New Zealand yamehirishwa kufuatia mvutano kuhusu tukio hilo. Waandaaji wa msako wa kila mwaka walikosolewa baada ya kutangaza kitengo kipya cha watoto kuwinda paka mwitu nchini New Zealand.

Vijana waliambiwa wasiue wanyama wa kufugwa, lakini walihimizwa vinginevyo waue paka wengi wa mwituni ili wapate zawadi ya NZ$250 (£124; $155). Tukio hilo lilileta shutuma kutoka kwa vikundi vya ustawi wa wanyama.

Siku ya Jumanne, Jumuiya ya Kuzuia Ukatili kwa Wanyama ya New Zealand ilisema kuwa imefarijiwa "mpango wa watoto ambao ulihusisha kuwapiga risasi paka mwitu" hautaendelea.

Mwakilishi alisema kuwa watoto, pamoja na watu wazima, hawataweza kutofautisha kati ya "paka mwitu, mpotevu au anayefugwa", kulingana na AFP. Pia kumekuwa na hofu kwamba paka wa nyumbani wanaweza "kunaswa kwenye mashambulii", mfadhili wa zamani wa uwindaji huo alikiambia chombo cha habari cha Stuff.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved