Msanii wa Mugithi na gengetone Peter Mwangi almaarufu Miracle Baby ametangaza kufufuka kwa uhusiano wake na mzazi mwenzake Carol Katrue.
Akithibitisha maendeleo hayo mapya Jumatano jioni, mtangazaji huyo wa zamani wa TV alifichua kwamba mama-mkwe wake alifanikisha maridhiano yake na mpenziwe.
Miracle Baby alimsifu mama ya mpenzi wake kwa usaidizi wake katika masuala yao ya uhusiano na akamtaja Mama Carol kuwa mama mkwe bora zaidi duniani.
"Mama, nataka kuchukua nafasi hii kukujulisha kuwa wewe ni mama mkwe bora ambaye najua upo kwenye kizazi hiki 🤗🤗 Mungu akubariki Kwa kusema nasi kwa maneno ambayo sitayasahau maishani mwangu," Miracle Baby alisema kupitia ukurasa wake wa Facebook.
Aliongeza, “Umenifanya nielewe kuwa sio sisi pekee tunaopitia mambo katika ndoa zote, lazima wakue na kushuka na sisi pia ni binadamu, lazima yatatutokea.”
Katika chapisho lake, mwimbaji huyo mwenye kipaji pia aliahidi kudumisha uhusiano wake na Carol Katrue, kumpenda, na kumlinda kila wakati.
“Asante
kwa mara nyingine tena utabaki kuwa mama mkwe wangu milele kwa sababu nitampenda
na kumlinda binti yako Carol Katrue kwa hali yoyote ile. Endelea kutuombea kwa
sababu ukituachalia na huku nje ni kutucheka panapotokea tatizo. wewe ndiye
mshauri bora wa ndoa Mungu akuzidishie siku zako hapa duniani Amina na amina.
Carol Katrue pia alithibitisha kurudiana kwake na baba wa mtoto wake mmoja akisema kuwa mamake alikuwa amezungumza nao.
Haya yanajiri siku kadhaa baada ya Carol Katrue kuthibitisha kuwa hawako pamoja tena baada ya kuchumbiana kwa miaka kadhaa.
Wawili hao walithibitisha kuachana kwao siku ya Ijumaa jioni wakati wakiwafahamisha mashabiki wao kwamba sasa kila mmoja anafanya kazi kivyake
. Katika taarifa yake, Carol Katrue alitangaza kuwa sasa yuko single na hafanyi kazi na mtu yeyote.
“Niko single!! Kwa bookings nidm mimi tafadhalisifanyi kazi na mtu yeyote au chini ya mtu yeyote,” Katrue aliandika kwenye Instagram.
Kwa upande wake, Miracle Baby aliweka wazi kuwa hayuko tena na mama wa mtoto wake mmoja na alitaka mtu yeyote anayemtafuta awasiliane naye moja kwa moja.
“Kwa yeyote aliyekuwa akinipigia simu kwa ajili ya show za Carol Katrue, hatupo pamoja tena!! asante,” Miracle Baby alisema.
Wawili hao wamekuwa wakichumbiana kwa miaka kadhaa sasa na wana mtoto mmoja pamoja.
Miracle Baby hata hivyo ana watoto wengine wanne na wanawake tofauti.