logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Msanii Miracle Baby amsifu mama mkwewe huku akitangaza kurudiana na Carol Katrue

Miracle Baby ametangaza kufufuka kwa uhusiano wake na mzazi mwenzake Carol Katrue.

image
na Samuel Mainajournalist

Dakia-udaku28 November 2024 - 08:46

Muhtasari


  • Miracle Baby alimsifu mama ya mpenzi wake kwa usaidizi wake katika masuala yao ya uhusiano na akamtaja kuwa mama mkwe bora zaidi duniani.
  • Mwimbaji huyo mwenye kipaji pia aliahidi kudumisha uhusiano wake na Carol Katrue, kumpenda, na kumlinda kila wakati.


Msanii wa Mugithi na gengetone Peter Mwangi almaarufu Miracle Baby ametangaza kufufuka kwa uhusiano wake na mzazi mwenzake Carol Katrue.

Akithibitisha maendeleo hayo mapya Jumatano jioni, mtangazaji huyo wa zamani wa TV alifichua kwamba mama-mkwe wake alifanikisha maridhiano yake na mpenziwe.

Miracle Baby alimsifu mama ya mpenzi wake kwa usaidizi wake katika masuala yao ya uhusiano na akamtaja Mama Carol kuwa mama mkwe bora zaidi duniani.

"Mama, nataka kuchukua nafasi hii kukujulisha kuwa wewe ni mama mkwe bora ambaye najua upo kwenye kizazi hiki 🤗🤗 Mungu akubariki Kwa kusema nasi kwa maneno ambayo sitayasahau maishani mwangu," Miracle Baby alisema kupitia ukurasa wake wa Facebook.

Aliongeza, “Umenifanya nielewe kuwa sio sisi pekee tunaopitia mambo katika ndoa zote, lazima wakue na kushuka na sisi pia ni binadamu, lazima yatatutokea.”

Katika chapisho lake, mwimbaji huyo mwenye kipaji pia aliahidi kudumisha uhusiano wake na Carol Katrue, kumpenda, na kumlinda kila wakati.

“Asante kwa mara nyingine tena utabaki kuwa mama mkwe wangu milele kwa sababu nitampenda na kumlinda binti yako Carol Katrue kwa hali yoyote ile. Endelea kutuombea kwa sababu ukituachalia na huku nje ni kutucheka panapotokea tatizo. wewe ndiye mshauri bora wa ndoa Mungu akuzidishie siku zako hapa duniani Amina na amina.

Carol Katrue pia alithibitisha kurudiana kwake na baba wa mtoto wake mmoja akisema kuwa mamake alikuwa amezungumza nao.

Haya yanajiri siku kadhaa baada ya Carol Katrue kuthibitisha kuwa hawako pamoja tena baada ya kuchumbiana kwa miaka kadhaa.

Wawili hao walithibitisha kuachana kwao siku ya Ijumaa jioni wakati wakiwafahamisha mashabiki wao kwamba sasa kila mmoja anafanya kazi kivyake

. Katika taarifa yake, Carol Katrue alitangaza kuwa sasa yuko single na hafanyi kazi na mtu yeyote.

“Niko single!! Kwa bookings nidm mimi tafadhalisifanyi kazi na mtu yeyote au chini ya mtu yeyote,” Katrue aliandika kwenye Instagram.

Kwa upande wake, Miracle Baby aliweka wazi kuwa hayuko tena na mama wa mtoto wake mmoja na alitaka mtu yeyote anayemtafuta awasiliane naye moja kwa moja.

“Kwa yeyote aliyekuwa akinipigia simu kwa ajili ya show za Carol Katrue, hatupo pamoja tena!! asante,” Miracle Baby alisema.

Wawili hao wamekuwa wakichumbiana kwa miaka kadhaa sasa na wana mtoto mmoja pamoja.

Miracle Baby hata hivyo ana watoto wengine wanne na wanawake tofauti.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved