logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ashtakiwa kuua mpenziwe baada ya kubainika aliwahi google ‘Naweza kuua binadamu haramu?’

Ty Vaughn, 31, kutoka jimbo la Texas nchini Marekani sasa anashtakiwa upya kwa mauaji ya mpenziwe baada ya awali uchunguzi wa kifo hicho kuonekana kama wa mtu kujitoa uhai mwenyewe.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Dakia-udaku13 March 2025 - 13:06

Muhtasari


  • Ty Vaughn, 31, sasa anashtakiwa upya kwa mauaji ya mpenziwe baada ya awali uchunguzi wa kifo hicho kuonekana kama wa mtu kujitoa uhai mwenyewe.
  • Hii ni baada ya kubainika kwamba alitafuta mtandaoni ili kujua madhara yalikuwaje kwa "raia halali" kumuua "mhamiaji haramu," kabla ya kifo cha Banos, kulingana na waraka huo.

Jamaa ashtakiwa kwa mauaji baada ya kupatikana ali'google jinsi ya kuua

MATOKEO ya historia ya ‘Google search’ kwenye simu ya mtuhumiwa yametumika kama Ushahidi mkuu katika kesi ya mauaji ya mwanamke ambaye alikuwa mpenzi wake.

Ty Vaughn, 31, kutoka jimbo la Texas nchini Marekani sasa anashtakiwa upya kwa mauaji ya mpenziwe baada ya awali uchunguzi wa kifo hicho kuonekana kama wa mtu kujitoa uhai mwenyewe.

Kwa mujibu wa jarida la PEOPLE, Vaughn alikamatwa na kushtakiwa kwa mauaji mnamo Ijumaa, Machi 7, kuhusiana na mauaji ya Januari ya Luis Banos mwenye umri wa miaka 27.

Mnamo Januari 14, maafisa wa polisi walijibu katika jumba la ghorofa huko Baytown baada ya mpiga simu 911 - ambaye baadaye alitambulika kama Vaughn - kudai kuwa amepata mchumba wake amekufa kutokana na jeraha la risasi, taarifa hiyo inasema.

Ndani, polisi walimkuta Banos akiwa amekufa na jeraha dhahiri la risasi na kumzuilia Vaughn kwa mahojiano.

"Wakati wote wa uchunguzi, Vaughn alitoa taarifa zisizolingana," polisi walidai. "Baadaye wapelelezi walibaini sababu ya kifo kuwa mauaji."

Vaughn sasa anashtakiwa kwa kumpiga risasi Banos usoni na bunduki na baadaye kuonyesha mauaji kama mtu wa kujitoa uhai.

Hii ni baada ya kubainika kwamba alitafuta mtandaoni ili kujua madhara yalikuwaje kwa "raia halali" kumuua "mhamiaji haramu," kabla ya kifo cha Banos, kulingana na waraka huo.

Nyaraka za mahakama zilizotajwa na ABC13 zinasema kwamba polisi waligundua kuwa aliwahi search kwenye mtandao wa Google, "Je, ninaweza kumuua binadamu haramu?"

Google

Kulingana na Fox 26, nyaraka za mahakama zinaonyesha Vaughn baadaye aliwaambia polisi kwamba mchumba wake "hakuwa na hadhi ya kisheria."

Polisi wanadai Vaughn alikuwa anajaribu "kupunguza au kudharau hadhi au thamani ya (Banos')," kwa kujadili hali yake ya uhamiaji, ripoti za San Antonio Express-News, zikinukuu hati ya kiapo ya upekuzi. Banos aliripotiwa kuwa mzaliwa wa Mexico.

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved