logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Thicky Sandra azungumzia kufanyiwa upasuaji wa kubadili muonekano wa mwili

Sandra anasema kwamba kwamba hana mpango wa kufanyiwa upasuaji kubadili umbile lake

image
na KEZIA ACHIENG'

Mastaa wako08 November 2024 - 09:55

Muhtasari


  •  Thicky Sandra amesema kuwa hana mpango wa kufanyiwa upasuaji wa urembo ili kubadilisha muonekano wake wa mwili.
  • Sandra pia alifichulia wafuasi wake anachofanya anapokumbana na haters ambao hukejeli maumbile yake.“

Mtayarishaji wa maudhui za dijitali Thicky Sandra amesema kuwa hana mpango wa kufanyiwa upasuaji wa urembo ili kubadilisha muonekano wake wa mwili.

 Kupitia kwenye chaneli yake ya YouTube, alizungumzia mada hiyo baada ya kuibuliwa na mmoja wa wafuasi wake kwenye mitandao ya kijamii wakati wa kipindi cha maswali na majibu kilichofanyika kwenye Instagram.

 Kulingana na Sandra, anaupenda mwili wake jinsi ulivyo. Aidha alifichua iwapo angefanyiwa utaratibu angepata moja inayolenga eneo la tumbo lake ili kupunguza ukubwa wa tumbo ila bado yuko sawa na jinsi tumbo lake ilivyo.

 “Ikiwa ni upasuaji wa kurekebisha mwili wangu na mimi mwenyewe, ningesema hapana. Ikiwa ningefanya kitu, ningefanya wood therapy ili kupunguza tumbo langu,”

 Aliendelea na kusema kitu kilicho kwa mwili wake ambacho angefikiria kubadilisha ni stretch marks ambazo anasema ziko sehemu mbalimbali mwilini mwake. Lakini hata kuhusu hilo alisisitiza kuwa bado hatafanya upasuaji.

 "Lakini nataka tu kuondoa stretch marks. Nina stretch marks nyingi sana kwenye mikono, tumbo, mapaja na nyash. Nisingefanya upasuaji lakini laser. Hicho ndicho kitu pekee ambacho ningetaka kifanyike kwa mwili wangu,” Sandra alisema kwenye video aliyowekwa kwenye chaneli yake ya YouTube.

Kuhusu ikiwa anapanga kupata watoto Sandra alisema kwamba anapanga kupata watoto lakini miaka kumi na zaidi kutoka sasa.

“Ndio, lakini labda baadaye maishani, kama miaka 10-15 kutoka sasa. Hapo ndipo ninapanga kupata watoto,” Sandra alisema. 

Sandra pia alifichulia wafuasi wake anachofanya anapokumbana na haters ambao hukejeli maumbile yake.“

Kadiri wanavyoniburuta chini ndivyo ninavyoinuka juu,” alisema.

Anasema ukiwa na haters inamaanisha unafanya kitu kizuri tofauti na kukosa haters kwani inamaanisha hakuna kile unachofanya.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved