logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Master J amepinga Kauli kwamba Diamond alimsaidia Harmonize kimuziki

Produsa maarufu wa muziki nchini Tanzania Joachim Marunda Kimaryo maarufu Master J amepinga kauli kwamba Diamond alimsaidia Harmonize.

image
na Japheth Nyongesa

Mastaa wako03 March 2025 - 12:06

Muhtasari


  • Master J kando na kuwa mutayarishaji wa muziki pia ni jaji katika shindano la kutafuta vipaji vya wasanii wa muziki nchini Tanzania maarufu kama Bongo Star Search.
  • Master J amewahi kupata tuzo ya 'Kili Music Award' mara mbili, mwaka 2004 na 2006.

Produsa maarufu wa muziki nchini Tanzania Joachim Marunda Kimaryo maarufu Master J amepinga kauli kwamba mwanamziki Diamond Platinumz alimsaidia Mwanamziki wa Konde Gang Harmonize kusimama katika tasinia ya muziki.

'Haya maneno ya kusema kuwa umemsaidia mtu, umemsaidia mtu saa ngapi, huyo Naseeb yeye watu ambao amewasainii, wote hawasaidii. Hizo ni shughuli za kibiashara tu. Mikataba ipo, mimi nitawekeza kiasi fulani," alisema Master J.

'Turekodi audio, tushooti video, na kufanya marketing and promotion. pesa zikipatikana wewe utachukua asilimia fulani na lebo itachukua kiasi fulani, msaada uko wapi? Ukitaka kuchomoka kabla ya kile nilichoeekeza hakijarudi, nilipe," alifafanua zaidi Muundaji huyo wa Muziki, Master J.

Kwa upande wake pia alieleza kwamba kumsaidia mtu kwenye tasnia ya mziki ni kumfanyia kazi mtu kisha umpe kazi na faida ya kazi hio ni yake lakini sio kuekeza nyote.

"Kumsaidia mtu ,ni kumsaidia kushooti video na audio kisha umwambie mzigo ndio huu hapa. Huo ndio msaada. Lakini hakuna msada kwenye lebo. Kwani mtu atoe hela yake bure. Mtu akusaidie milioni 50 au milioni 100, bure," alisema Mater J kwa kutilia shaka.

Master J kando na kuwa mutayarishaji wa muziki pia ni jaji katika shindano la kutafuta vipaji vya wasanii wa muziki nchini Tanzania maarufu kama Bongo Star Search.

Master J amewahi kupata tuzo ya 'Kili Music Award' mara mbili, mwaka 2004 na 2006. Master Jay ana uwezo mkubwa sana wa utengenezaji wa muziki. Anamiliki studio tatu tofauti, moja ya muziki wa kwaya, moja ya Bongo fleva na nyingine ya muziki wa Dansi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved