Kwa kweli hamna njia wala siku na saa mabazo wanandoa wanapswa kufanya ngono cha muhimu ni kuwa wote wamo na hisia za kufanya hayo.
Wengi wanapenda ngono na kisha unapata kuwa mwenzie hana haja na ngono siku hiyo je unapswa kufanya nini, usitie shaka bali majibu yote utayapata kwenye makala haya, ya ni mara ngapi wanandoa wanapswa kufanya ngono kulingana na wanasayansi.
Lakini kama wataka kuongeza mchezo wako wa kitandani hamna shida na hilo, kwa kweli kuongeza mchezo wako kunaweza fanya uridhke katika uhusiano wako.
Biblia haituambii ni mara ngapi wanandoa wanapaswa kufanya ngono, lakini inatuambia kwamba wanandoa wanapaswa kujizuia tu wakati uamuzi wao ni wa pamoja. Wakorintho wa Kwanza 7: 5 inatuambia, "Msinyimane isipokuwa mmepatana kwa muda, ili mpate faragha kwa kusali; mkajiane tena, Shetani asije akawajaribu kwa kutokuwa na kiasi kwenu." Kwa hivyo, kuwa na kiasi ni "sheria" ya ni mara ngapi wanandoa watakuwa na ngono. Sheria ni kuwa kujisuia lazima kuwe kwa makubaliano, na kwamba hata wakati umekubaliana, ni lazima tu kuwe kwa muda mfupi.
Kulingana na wanasayansi wengi kufanya ngono mara moja kwa wiki hakuwezi changia kuvinjika kwa ndoa wala uhusiano kati ya wapenzi wawili.
Haya hapa maswali ambayo wanandoa wanapaswa kujiuliza kuhusu ngono;
1.Je kwanini kufanya ngono kila mara ni jambo kubwa
Wengi husema kuwa kufanya ngono kila mara ni kuridhisha mwenzio katika uhusiano wenu, lakini kufanya ngono kila mara si jambo kubwa, hii ni kwa sababu kuna wengi ambao wamo katika uhusiano wa kimapenzi na wana furaha ilhali hawafanyi ngono wala chochote.
Ni jukumu lako wewe kufanya ambacho mpenzi wako anakipenda na wote mko na furaha katika uhusiano wenu na wala si kila mara kufanya ngono.
Kwa wapenzi ambao huwa wanajawa na furaha kwenye uhusiano wao kwa ajili ya ngono huwa wanapendana sana kwa maana kila mmoja ameridhika kwa hisia zake.
2. Je unapaswa kupanga siku ya kufanya ngono?
Kuweka siku za kufanya ngono na mke au mume wako si jambo ambalo unapaswa kufanya, lakini kama umeshikana na kazi, watoto au unafanya kazi ya usafiri unaweza panga siku za kufanya hayo kwenye kalenda yako ya mwezi.
Pia unaweza kumshangaza mpenzi wako usiku mmoja kwa kutenga wakati wenu bila kusumbuliwa na yeyote na kisha kumuonye mahabara yenu na mapenzi.
3. Kama sina hisia za kufanya ngono kama mwenzangu
Ngono haipaswi kuzuiwa au kulazimishwa. Ikiwa mwanandoa mmoja hataki kufanya ngono, mwenzi mwingine anapaswa kukubaliana naye. Yote ni jambo la maelewano. Lazima tukumbuke kwamba miili yetu ni ya washirika wetu, kama 1 Wakorintho 7: 4 inatuambia, "Mke hana amri juu ya mwili wake, bali mumewe; vivyo hivyo mume hana amri juu ya mwili wake, bali mkewe." Kwa wazi, "maelewano ya ngono" katika ndoa lazima yawe ya busara. Ikiwa mwenzi mmoja anatamani ngono kila siku, na mwenzi mwingine mara moja kwa mwezi au chini, wanapaswa kwa upendo na dhabihu kukubaliana. Uchunguzi unaonyesha kwamba kuzingatia kila umri wa miaka, wanandoa wa kawaida wanajamiiana mara 2 kwa juma.
4.Jinsia ngapi kila mtu mwingine anafanya, ingawa?
Wanandoa w miaka 30 mpaka 39 hufanya ngono mara 86 kwa mwaka kulingana na uchunguzi, aslimia 28% kati ya wanandoa 45 hufanya ngono mara moja kwa wiki.
Kulingana na uchunguzi wanandoa wa miaka wa 19 hadi 29 hufanya ngono mara 112 kwa mwaka. pia wanandoa hawapaswi kujiuliza wanandoa wenzao wanafanya ngono mara ngapi katika ndoa yao.
5. Je kama namba yangu ya ngono haiko sawa na wanandoa wale wengine?
Kufanya ngono si kwa ajili ya mwenzia amefanya wala anafanya bali hisia zenu zikiamka mnapaswa kufanya ngono wakati wowote mahali popote kama nyinyi ni wanandoa na wala si wachumba.
Kama namba ya mwezio haikufurahishi katika ngono cha muhimu ni kuwa muweze kuelewana na kuzungumza kama ni kuongeza siku za kufanya ndoa au kupunguza, wanandoa wakitaka kufanya ngono lazima wawe katika makubaliano.
Cha muhimu kati ya wanandoa ni mawasiliano yao kuhusu ngono na mawaidha ya kila mmoja kutiliwa maanani. je maoni yako ni yapi kuhusu wanandoa wanapaswa kufanya ngono mara ngapi?