Kufutwa kwa watangazaji wa homeboyz radio wiki jana, kulijiri saa chache baada ya kutoa maoni mabaya kuhusu mwanamke huku maoni yao yakizua mjadala mkali mitandaoni.
Majadiliano ya watatu hao yalionekana kupendekeza kwamba mwanamke aliyesukumwa nje dirisha la ghorofa ya 12 baada ya kukataa ngono na mpenzi wake anapaswa kulaumiwa kwa kitendo hicho.
Baada ya video ya onyesho kuwekwa mtandaoni, watatu hao walisitishwa na kufutwa kazi, Kampuni ya Bia ya Afrika Mashariki ilivuta matangazo yao kutoka kwa kipindi hicho.
Mamlaka ya Mawasiliano ya Kenya iliingilia kati kutoza faini ya milioni 1 kwa homeboyz radio(ambayo inamilikiwa na Radio Africa Ltd) na kusitisha programu hiyo kwa miezi sita.
Hii si mara ya kwanza kwa vyombo vya habari vya Kenya kupeperusha mambo ya dharau juu ya wanawake.
Lakini swali kuu ambalo wengi tumasahau ni kwamba mwanamume anapoamua kumtupa mwanamke kutoka katia ghorofa ya 12 alikuwa anafikiria nini
Pia hamna haja ya kuuliza kwanini mwanamke huyo alikuwa na mwanamume huyo,swali ni je mwanamume huyo alikuwa na akili timamu?
Wanamitandao wengi walitoa maoni tofauti huku baadhi ya wengine wakiwakashifu watangazaji hao kwa ajili ya maoni yao.
Kuna baadhi ambao walisema kwamba wanaume ambao hutoa maoni mabaya kuhusu wanawake ni wanyanyasaji.
Je maoni yako ni yapi kuhusu wanaume ambao hutoa maoni mabaya kuhusu wanawake?