logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Msanii wa nyimbo za injili Size 8 kutawazwa kuwa mhubiri

Atakuwa mhubiri katika kanisa la JCC Thika.Pia alimshukuru mumewe kwa kumshika mkono katika

image
na Radio Jambo

Football08 December 2021 - 14:15

Muhtasari


  • Msanii wa nyimbo za injili Size 8 kutawazwa kuwa mhubiri

Msanii wa nyimbo za injili Size 8 atatawazwa kuwa mhubiri JUmapili Desemba 12.

Kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram msanii huyon alitangaza hafla hiyo na kusema kwamba ni jambo lenye hisia kwake.

Atakuwa mhubiri katika kanisa la JCC Thika.Pia alimshukuru mumewe kwa kumshika mkono katika safari yake.

Nitawekwa wakfu kuwa mhudumu wa neno la Mungu, mtumishi wa Mungu aliye juu Jumapili hii na waaaa hiii ni emotional😭😭😭😭 Mungu si mtu hata aseme uongo

Anamchagua yeyote na kuwabadilisha ili wamtumikie.... Maisha yangu ni sawa na sinema kutoka kwa ulimwengu wa kidunia hadi kwa mtumishi aliyewekwa rasmi wa Mungu 😭😭😭 muone Mungu......

Nehema za Mungu ni za kweli.... .. Nilizaliwa mara ya pili 2013 nilianza safari ya muziki wa Injili, miaka mitano baadaye 2018 nilisoma shule ya Biblia na kuhitimu na sasa miaka 8 baadaye 2021 naenda kuwekwa wakfu 😭😭😭😭 muone Mungu...

Na kwa Mungu awe utukufu kwa neema yake tu, nguvu zake na roho yake kupitia kwa mwanawe Yesu Kristo imetokea KWA WAKATI WA MUNGU HUFANYA KILA KITU KIZURI!!!

KWA mume wangu @djmokenya asante kwa kuniruhusu kwenda kumtumikia Mungu na kwa Mchungaji na washauri wangu Pastor Kelvin na Jacky Ephraim Mungu awabariki nyote.....

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved