logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Hakuna mabadiliko yoyote katika tarehe za mitihani ya KCPE na KCSE- KNEC

KNEC imesema habari zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu kuahirishwa kwa mitihani ya mwaka ujao si za kweli.

image
na Radio Jambo

Habari09 December 2021 - 05:45

Muhtasari


• KNEC imesema habari zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu kuahirishwa kwa mitihani ya mwaka ujao si za kweli.

Watahiniwa wa darasa la nane wakalia mtihani wa KCPE

Baraza la mitihani la Kenya (KNEC) limepuuzilia mbali madai ya kuahirishwa kwa mitihani ya kitaifa ya darasa la nane (KCPE) na kidato cha nne (KCSE).

Kupitia kwa taarifa iliyotolewa na mkurugenzi mtendaji David Njengere siku ya Alhamisi, KNEC ilisema habari zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu kuahirishwa kwa mitihani ya mwaka ujao si za kweli.

KNEC imesema hakuna mabadiliko yoyote ambayo yamefanywa katika tarehe za mitihani ya kitaifa ya KCSE na KCPE.

"Tunataka kuwafahamisha washikadau wote husika kwamba hakuna mabadiliko yoyote katika tarehe za mitihani ya kitaifa ya KCPE na KCSE" KNEC ilisema.

Watahiniwa wa KCPE 2021/22wanatarajiwa kuanza mtihani wao mnamo Machi 7, 2022 na kutamatika tarehe Machi 9.

Mtihani wa KCSE 2021/22  utang'oa nanga mnamo Februari 22, 2022 na kuendelea hadi tarehe mosi mwezi Aprili, 2022.

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved