logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Uchumi wa Kenya katika hali mahututi kwa sababu ya sera mbovu, sio maandamano - Raila

Raila Odinga amesema uchumi uko katika hali mbaya sababu ya sera mbovu za serikali.

image
na

Grafiki25 July 2023 - 08:32

Muhtasari


• Raila Odinga amesema uchumi uko katika hali mbaya si kwa sababu ya maandamano yaliyoandaliwa na muungano huo bali sera mbovu za serikali.

Kinara wa upinzani Raila Odinga

Kiongozi wa Azimio la Umoja Raila Odinga amesema uchumi uko katika hali mbaya si kwa sababu ya maandamano yaliyoandaliwa na muungano huo bali sera mbovu za serikali.

Akihutubia vyombo vya habari vya kimataifa Jumanne, Raila alisema kuwa serikali imekuwa ikimlaumu Rais mstaafu Uhuru Kenyatta ilhali wamekopa zaidi ya alivyokopa.

“Unalaumu utawala wa Rais wa Awali Uhuru Kenyatta kwa hali ya uchumi  nchini ilhali aliondoka serikalini mwaka jana Septemba,” akasema.

Kiongozi huyo wa chama cha ODM, aliongeza kuwa serikali hii imehudumu kwa muda wa miezi 10 tayari na bado lalama zao ni kuwa Rais mstaafu Kenyatta alikuwa akikandamiza hatua zao za kujaribu kufufua Uchumi.

"Sasa tuko Julai na mmeendesha serikali hii kwa miezi 10 iliyopita. Tulitarajia kuona mabadiliko fulani ndani ya muda huo."

Wakati wa kuapishwa baada ya kuibuka akama washinda wa uchguzi wa mwaka 2022, Naibu Rais Gachagua alibainisha kuwa walikuwa walirithi serikali iliyodorora kutoka kwa Rais mstaafu Uhuru Kenyatta.

Alibainisha kuwa kuna changamoto ya upatikanaji wa fedha za maendeleo kwa sababu kiasi kinachokusanywa na Hazina ya Taifa kinatumika kulipa mishahara na kulipa madeni.

"Nataka kurudia ili tena. Tumerithi uchumi uliodorora na tuna kazi ya kufanya kugeuza uchumi wa nchi hii na tutakuwa na wito kwenu nyote mtuvumilie kwa sababu si  kazi rahisi," Gachagua alisema.

Raila amekuwa kimya na hakujitokeza wakati wa maandamano akidai kuwa alikuwa akiugua homa na hakuweza kujitokeza na kujinga na wafuasi wake waliolekea mitaani kuandamana kwa sababu ya gharama ya juu ya hali ya maisha.

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved