Picha kwa hisani ya: elcrema.com
Kijana mmoja kwa jina Antony Otieno mwenye umri wa miaka 20 kutoka katika kijiji cha Nyawara amejitoa uhai kwa madai ya kuachwa na mamake aliyeelekea Nairobi kazini.
Inadaiwa kuwa kijana huyo alimtaka mamake kujenga kabla ya kurejea Nairobi anakotafuta riziki lakini mamake alipuuza agizo la mwanawe na kuwaacha na nyanyao swala lililo mkasirisha marehemu na kuamua kujitia kitanzi.
Kulingana na baadhi ya wanafamilia kijana huyo alionekana mwingi wa mawazo hapo jana na pindi alipomaliza kula chakula cha jioni alitoweka nyumbani kabla ya mwili wake kupatikana ukininginia leo asubuhi kwenye mti wa maembe.
Akithibitisha kisa hicho chifu wa eneo hilo David Otieno amewataka wazazi kuwapa ushauri wanao hasa wanapoonekana kusongwa na mawazo.

