Photo source: nairobinews.co.ke
Polisi hapo jana wamewaua kwa kuwapiga risasi majambazi wanne katika mtaa wa kifahari wa Loresho hapa Nairobi.
OCPD wa Gigiri Vitalis Otieno anasema wanne hao waliofumaniwa wakati wakiiba bidhaa boma moja mtaani hapo walipatikana na bastola na risasi nne.
