logo

NOW ON AIR

Listen in Live

VIDEO: Tazama mwanahabari Yusuf Juma akisoma habari moja kwa moja

VIDEO: Tazama mwanahabari Yusuf Juma akisoma habari moja kwa moja

image
na

Habari01 October 2020 - 14:49
Mwanahabari wa Radio Jambo, Yusuf Juma,  bila shaka ni mmoja wa wanahabari bora zaidi humu nchini.

Ufasaha wake katika lugha ya taifa na ubabe wake ni mojawapo tu ya sifa ambazo zimejaa kwenye hazina lake, ambalo limemfanya kuwa nyota linalong'aa katika wingu la sanaa ya uanahabari kila uchao.

Yusuf Juma anayetambulika kwa jina la utani kama 'YJ',  anatambulika zaidi miongoni mwa mashabiki wa Radio Jambo kwa sauti ya kina, huku wengi wao wakiisifia kama sauti iliyo na uwezo wa kutoa nyoka pangoni. Licha ya kusoma habari kila baada ya saa na nusu saa kila siku ya wiki, kutoka mida ya saa kumina mbili hadi saa nne, mwanahabari huyu wa miraba minne pia ana kitengo cha 'Kiswahili sio mdomo wetu'.

Also read:

Kupitia kitengo hiki, zaidi ya wakenya millioni 10 hupata fursa ya kujifunza maneno au majina mapya ya Swahili.

Lakini je, ni yepi haswa huendelea wakti wa usomaji habari?.

Kupitia mtandao wake wa Youtube bwana YJ alijibu swali hilo baada ya kuchapisha kanda yake, huku akionesha ubabe wake nyuma ya kipaza sauti,.

Tazama mwanahabri huyu akisoma habari moja kwa moja kutoka studio za Radio Jambo.

&feature=youtu.be


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved