logo

NOW ON AIR

Listen in Live

SIAYA: Gavan Rasanga Apiga Marufuku Uridhi Wa Wajane

SIAYA: Gavan Rasanga Apiga Marufuku Uridhi Wa Wajane

image
na

Habari01 October 2020 - 16:27
rasanga
Gavana wa kaunti ya Siaya Cornell Rasanga amepiga marufuku utamaduni wa kuwaridhi wajane kwa lengo la kupunguza maambukizi ya ugonjwa wa ukimwi.

Rasanga alielezea kuwa kusheheni kwa ugonjwa wa ukimwi katika kaunti ya Siaya kumechangiwa na utamaduni wa kuwaridhi wajane.

Aliongezea kuwa anapania kutenda fedha ambazo zitatumika kama hazina ya wajane ili kuwasaidia kufungua biashara ili kujikimu kimaisha na kuwasaidia kujiepusha na utamaduni wa kuridhiwa kwa mjibu wa usaidizi.

Aidha haya yanajiri baada ya baraza la kuthibiti ugonjwa wa ukimwi kubaini kuwa kaunti ya Siaya ni ya tatu nchini katika usabazaji wa ugonjwa wa ukimwi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved