logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwana Wa Miaka 15 Abakwa Na Kujeruhiwa Na Mpenzi Wa Mamake

Mwana Wa Miaka 15 Abakwa Na Kujeruhiwa Na Mpenzi Wa Mamake

image
na

Habari01 October 2020 - 20:37
Mtoto mmoja wa umri wa mia kumi na tano anaendelea kuuguza majeraha baada ya kunajisiwa na kujeruhiwa na mpenzi wa mamake katika kijiji cha Siyenga kata ya seregeya eneo bunge la likuyani.

Akizungumza na wanahabari mwathiriwa ambaye ni mwanafunzi katika shule ya msingi ya siyenga amesema mshukiwa David Lugalia almaarufu mia mbili amekuwa akimhadaa kwa shillingi ishirini kabla ya kumtendea unyama huo na baadaye kumuonya dhidhi ya kumueleza yeyote kabla ya kufumaniwa na mchungaji wao akitekeleza kitendo hicho.

Kisa hiki kimedhibitishwa na afisa wa watoto katika kaunti ndogo ya likuyani bi Milcah Chelagat Sitienei ambaye amesema polisi wanamsaka mshukiwa ambaye amekimbilia mafichoni kwa sasa.

-Brian Ojamaa

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved