logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mauaji ya Wambui: Polisi kumuachilia huru Joseph Kori

Mauaji ya Wambui: Polisi kumuachilia huru Joseph Kori

image
na

Habari02 October 2020 - 00:34
Joseph Kori ambaye ni mume wa mwendazake Mary Kamangara, Alhamisi ilikuwa siku ya kueka katika kumbukumbu zake za maisha hii ni baada ya kutolala korokoroni kwa maana aliweza kuachiliwa huru.

Alihusika na mauaji ya mke wake wiki tatu zilizopita huku mpenzi wake akiwa ni yeye aliyemuua Mary Kamangara mke wa Kori.

Mpenzi wake Kori Judy Wambui bado yumo mikononi mwa polisi katika kituo cha polisi cha Muthaiga. Familia ya Wambui iliweza kusema kuwa walikuwa wanangoja Kori aachiliwe ili waweze kumzika Wambui.

"Katika uchunguzi ambao ulifanyika na kuonekana kuwa Kori hakuweza kuhusika katika mauaji ya mke wake, sisi kama familia tuliamua kumngoja aweze kuachiliwa huru ili aweze kumzika mke wake, nyumbani kwake Mweiga kaunti ya Nyeri," Bi Esther Kamangara alisema.

Februari, 13, Mahakama ya Kiambu iliweza kuambia sekta ya DCI iweze kuwaeke wawili hao korokoroni, pamoja na dereva ambaye alikuwa amembeba mwendazake Mary, kwa siku 14 ili wachunguzi waweze kuendeleza na uchunguzi wao.

Awali Joseph Kori aliweza kuambia mahakama imuachilie kwa dhamana kwa maana uchunguzi haukuweza kuonyesha kuwa alihusika katika mauaji ya mke wake.

Mkuu wa DCI George Kinoti aliweza kuambia Inspekta John Wahome aweze kuongoza uchunguzi wa mauaji hayo, wakati wa mauaji hayo uchunguzi ulionyesha kuwa Kori alikuwa katika kaunti ya Kajiado maeneo ya Ngong.

Aliweza kutoka maeneo hayo saa tatu usiku.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved