logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Diamond Platnumz na babake wakutana na kuzima tofauti zao

Diamond Platnumz na babake wakutana na kuzima tofauti zao

image
na

Habari02 October 2020 - 01:14
Msanii na staa mkubwa Afrika Diamond Platinumz ameweza kukutana katika redio ya Wasafi FM na babake na kuonekana kuzima tofauti zao za awali.

Mzee Abdul alimtaliki mkewe miaka ya awali kijana huyu akiwa kidato cha kwanza. Naseeb alitangulia kwa kusema kuwa ubaridi unaonekana kati yao na baba mzazi umechochewa na kutokua pamoja kwa kipindi kirefu.

“Kiukweli siwezi kusema nina ukaribu na mzee. Hatujakuwa na bond kubwa naye ila mimi sina matatizo naye…tukiwa kuna issue tutakutana naye tuongee” Diamond alisema katika mahojiano.

Kwa upande mwingine anaona kuwa babake anamweka katika kicheko kwa watu wengi hususan wapinzani wake anapoonekana kama hamsaidii mzazi.

Babake alimwomba msamaha na wote kuonekana wameridhiana katika mazungumzo yao

“Kama nimekukosea naomba unisamehe na ujaribu kuangalia utanisaidia vipi mimi babako.”

Diamond alionya kuwa kuna baadhi ya vyombo vya habari vinavyomtumia babake kwa maslahi yao na hawamsaidii. Mkali huyu wa kibao kipya The one  alimaliza kwa kuomba msamaha.

“Well mimi siwezi kusema nina  matatizo na babangu. Naamini utofauti wake na mama unafanya tuwe hatuna ukaribu…Naomba anisamehe pia kwa sababu sijui akiwa na mama walikosana kwa misingi gani.”


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved