logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ilikuaje: Harrison Mumia asimulia mbona hamuamini mungu

Ilikuaje: Harrison Mumia asimulia mbona hamuamini mungu

image
na

Michezo02 October 2020 - 01:42
Mgeni wake Massawe Japanni leo katika kitengo cha Ilikuaje, alikuwa ni bwana Harrison Mumia ambaye anajulikana kwa kutomuamini mungu na ambaye pia ni rais wa wasiomuamini mola.

Harrison alidai kuwa alilelewa katika famili inayomcha mungu lakini anakiri kuwa 'alifunguka macho' pindi alipojiunga na chuo kikuu.

Anasema kuwa mungu hayupo na kuwa ni mawazo tu ya binadamu, isitoshe anaamini kuwa kama wa Afrika twapaswa kuchambua bibilia kwani lina makosa chungu nzima.

Nililia familia ambayo baba na mama walikuwa wakristo  kabla ya kubadilika nilipofika chuo kikuu.

Kila anayenijua anafikiri kuwa nimerogwa ama kuna kitu kibaya nami lakini nataka kusema kuwa sisi atheists ni watu wako sawa. Sinywi pombe, situmii madawa na nina kazi lakini ikifika kwa mungu simuamini.

Mamangu aliniombea sana na hadi sasa bado huniombea na ile iko ni kuwa maombi hayafanyi kazi. Babangu pia aliniombea lakini mda ulifika na akanielewa. Alisema Harrison.

Harrison anasema kuwa kinyume na jinsi wengi wanavyoamini, wanaoamini mungu yuko ndio wamepotea huku akisisitiza wasiomuamini mungu ndio watakao okoa Kenya.

Harrison alifichua kuwa yeye na wenzake hukutana Jumamosi ya mwisho ya kila mwezi kuzungumzia maswala yanayowakumba. Alisema kuwa kuna mipango yao kuweka mikutano yao siku ya Jumapili ili iwe kama dini la tatu.

Atheists in Kenya ina wanachama 600 ambao wamejiandikisha lakini tuna wafuasi elfu kumi. Tunataka kuweka mikutano yetu siku ya jumapili kwani tunataka kuwapa wakenya chaguo. 

Cha kushangaza ni kuwa Harrison huskiza nyimbo za injili lakini zenye mdundo kama wa lingala. Licha ya kutomuamini mola anadai pia ana imani shetani pia hayupo.

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved