logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Robert Alai apondwa mtandaoni baada ya DCI kumwanika na picha ya ‘mhalifu’

Robert Alai apondwa mtandaoni baada ya DCI kumwanika na picha ya ‘mhalifu’

image
na

Habari02 October 2020 - 02:00
Robert Alai
Mwanablogu Robert Alai ndiye hujipata akiwafanyia watu kejeli mtandaoni kupitia  maoni yake ambayo  wakati mwingine huwa ya kikatili . Lakini leo amejipata amevalia kiatu tofauti cha kufanyiwa kejeli hizo na wakenya mtandaoni baada ya idara ya DCI kutoa picha yake  akiwa amebeba bango lenye  maelezo yake baada ya kukamatwa kwa kueneza mtandaoni picha za miili ya polisi waliouawa huo wajir katika shambulizi la kigaidi .

Alai amejipata matatani baada ya tume ya Uwiano na maridhiano kutangulia kumsihi aziondoe picha hizo katika mitandao ya kijamii lakini akapuuza . Katika kinachothibitisha msemo aliye juu mngoje chini ,Alai hajaonewa huruma na wengi wanaomponda huku wengine wakimrejesha nyuma kumkumbusha kuhusu ukosoaji wake mkali dhidi ya kinara wa ODM  Raila Odinga .

Hata hivyo baadhi ya wanamtandao hawajapendezwa na hatua ya polisi kuiweka nambari ya simu ya Alai hadharani katika kibango alichopigwa nacho picha .

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved