Mtindo huu ukikumbuka ulianzishwa na chuo kikuu cha Mlima Kenya (Mount Kenya University) kabla ya chuo kikuu cha Kenyatta kujenga lango la kisasa na lenye gharama ya juu.
Isitoshe, mradi huo wa lango la chuo kikuu cha Kenyatta, ulijumuisha majengo matatu mapya ambayo iliwagharimu mamilioni ya pesa.
Miaka kadhaa baadae, mtindo huu umegeuka na kuwa kama mashindano kati ya vyuo hivo huku kila mmoja akitaka kuonesha ubabe wake katika uwanja wa ubunifu.
Vyuo vingine vikuu ambavyo vimefuata mtindo huu wa kisasa ni chuo kikuu cha Kilimo na Teknolojia cha Jomo Kenyatta (JKUAT, Juja), chuo kikuu cha Pwani, chuo kikuu cha Egerton, chuo kikuu cha Kabianga, Kericho, na mengineo.
Tazama picha za baadhi ya vyuo hivi.
