logo

NOW ON AIR

Listen in Live

''Nitawalea watoto wa Mbosso,'' Binti afunguka mwanzo mwisho

''Nitawalea watoto wa Mbosso,'' Binti afunguka mwanzo mwisho

image
na

Habari02 October 2020 - 03:54
mbosso
Binti wa humu Kenya jina lake Munira mkaazi wa Mombasa alifunguka wazi bila aibu kuwa, anamtamani sana mwanamziki wa Bongo, Mbosso. Amini usiamini, Munira alisema kuwa hatawacha kumtamani Mbosso mpaka wakati ambao atamkubali na kumpenda anvyo mpenda.

Munira alisafiri mpaka nchini Tanzania ili amuone Mbosso na kusema kuwa yuko tayari kufanya lolote lile mradi ampate Mbosso.

Katika mahojiano na vyombo vya habari, Munira alisema,

''Nampenda. Kuna wanaume wengi sana wanataka kunioa huku Kenya lakini siko tayari. Nilikuja kumtafuta Mbosso na niko tayari kufanya lolote lile. Nampenda sana. Nilianza kumpenda tangu wakati alikuwa kwenye bendi ya YA MOTO. Niliuza simu yangu ndipo niweze kusafiri mpaka Tanzania.'' Munira alisema.

 Vilevile, alizidi kusema kuwa ,iwapo Mbosso hatamkubali, atakunywa sumu na iwapo atamkubali, basi atampenda yeye pekee yake na kuwalea watoto wake Mbosso.

Munira alisema kuwa, Mwanzamziki huyu alisisitiza sana arudi nyumbani na hata kumpa shillingi elfu 10,000 za Tanzania lakini yeye hataki.

''Mwishowe, nimekutanana na yeye na aliniambia atanipea fare ya kurudi nyumbani lakini mimi siko tayari kurudi nyumbani. Alinipea shillingi 10,000 ya nauli lakini sitaki.''

Mbosso alipoambwa afunguke kuhusu yaliyotokea, alisema kuwa amekwisha tulia na mama ya mtoto wake na hataki mambo mengi.

''Siwezi mhukumu kwa yale aliyosema. Nina familia na watoto. Kuwa na uhusiano wa kimapenzi na binti mwingine ni upuzi tu. Nataka arudi nyumbani.'' Mbosso alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved