logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Diamond, Tanasha wanahatarisha kufungwa jela Tanzania

Diamond, Tanasha wanahatarisha kufungwa jela Tanzania

image
na

Dakia-udaku02 October 2020 - 04:07
Screenshot_from_2019_11_17_11_31_06__1573979495_12289
Staa na nguli wa muziki Afrika Diamond Platnumz na Tanasha Donna huenda wanahatarisha kutiwa nguvuni na mamlaka nchini Tanzania katika kipengele kipya cha kuhalalisha ndoa.

Nchi jirani ya Tanzania inasukumia kuwepo na urasmi wa ndoa kati ya raia wao.

Diamond na Tanasha ni miongoni mwa wanandoa nchini humo ambao hawajaona rasmi.

https://www.instagram.com/p/B4hsCzKAXnU/

Serikali ina mtazamo kuwa mtindo wa wanandoa kuishi chumba kimoja bila kuoana rasmi ni chanzo cha watoto wanaorandaranda mitaani.

Ndoa hizi zikivunjika, watoto hupata tabu kubwa sana na wengi huishia kuombaomba kwenye vichochoro.

Andrea TSele alitangaza kuwa wanandoa kama hao wakamatwe na kutiwa nguvuni ili wajue ubora wa kufunga ndoa.

TSele alikuwa akizungumza katika kata ndogo ya Mavanga jimbo la Ludewa Njombe .

Kinachomkera TSele ni wanaume wanaowakimbia wamama baadaye ya kuwatunga ujauzito.

" Na hawa watu wanastahili watiwe mbaroni kwa kuwa hawataki kuhalalisha ndoa ilihali wanataka kuishi kama mume na mke..." Tsele.

Tsele alihofia sana uongezeko wa watoto wanaorandaranda mitaani.
Zari The Boss Lady amenukuliwa kusema kuwa Diamond hatoi usaidizi unaotakiwa kwa watoto wao.
Hapo awali, Zari alimuonya Tanasha kuwa ajitayarishe kulea mtoto peke yake.
Inadaiwa kuwa Tanasha na Diamond wanaishi katika chumba kimoja ila hawajaona.

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved