logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mourinho: Mashabiki wa Arsenal, Chelsea na United watoa hisia zao

Mourinho: Mashabiki wa Arsenal, Chelsea na United watoa hisia zao

image
na

Habari02 October 2020 - 04:09
Klabu ya North London na anakochezea nahodha wa Harambee Stars, Victor Wanyama, Tottenham imemteua Jose Mourinho kama kocha mpya.

Mourinho ambaye awali alikuwa mkufunzi wa Chelsea na pia Manchester United kwenye ligi kuu ya Uingereza, anajiunga na Spurs masaa machache tu baada ya kutimuliwa kwake Mauricio Pochettino.

Pochettino alifutwa kazi jana baada ya miaka mitano ya kuingoza klabu hiyo ya North London. Mourinho amekua bila ya ajira baada ya kufutwa kama meneja wa United Disemba mwaka 2018.

Pochettino aliiongoza Spurs kumaliza katika nafasi ya nne bora katika misimu minne kati ya mitano aliyokuwa meneja wa klabu hiyo na vilevile fainali yao ya kwanza la ligi ya mabingwa mwaka wa 2018/19.

Akizungumza baada ya uteuzi wake, Mourinho alisema,

"Nimefurahia kuungana na Klabu iliyo na urithi mkubwa na wafuasi wenye shauku kubwa. Ubora katika kikosi na taaluma zote zinanifurahisha. Kufanya kazi na wachezaji hawa ndio kilichonivutia. ”
Uteuzi wake Mourinho wajia wakti ambapo mashabiki wa Arsenal walikuwa wanammezea mate baada ya kumshtumu maneja Unai Emery. Unai amekuwa na kipindi kigumu kwani wanabunduki hawajakuwa wakionesha mchezo bora.
Kulikuwa na tetesi kuwa Mourinho angependa kurudi katika ligi kuu ya Uingereza na timu nyingine na wengi walidhania kuwa huenda akajiunga na Arsenal.
Mashabiki hao hao wa Arsenal sasa wamekimbia kwenye mitandao ya kijamii kutoa hisia zao, huku wakiungana na mashabiki wa Man United na Chelsea ambao walimjua Mourinho vyema.
Ifuatayo ni baadhi ya hisia zao.
Mohamed: We missed you me specialist 😒

Son will be a left back , Harry Kane will be the best defender in the EPL .. 😂🤣

Samuel LFC: Despite that I don’t feel appointing Jose Mourinho is a good move for Spurs, I’m already dreading the away fixture for the inevitable ‘parking the bus’ tactic on the 11th of January.
King Nonny: The best thing that happened is Mourinho getting a Job so his Fans can leave Man Utd alone. Y"all Follow him to Tottenham & support your master in peace. Need all that Negativity out of this Club
Benjamin: Spurs will regret the Mourinho appointment. He'll give a couple of youths a chance, but he'll always want to spend more money on big players, which Levy doesn't do. No doubt about it - this is another Utd short term appointment because they want trophies fast.
KikoCfc: Jose doing his job man destroyed man United and made them mid table team now time to send spurs champions ship This is football Heritage


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved