Maribe na Jowie walichumbiana mwaka uliopita na walikuwa wanapanga kufunga pingu za maisha. Hata hivyo, mwezi Septemba mwaka huo huo wawili hao walitiwa mbaroni kufuatia kifo chake Monica Kimani.
Baada ya kukaa wiki chache korokoroni, Maribe aliachiliwa kwa dhamana, huku Jowie mtuhumiwa mkuu akarushwa katika gereza la Kamiti.Jowie na Maribe walikuwa wakichapisha picha zao katika akaunti zao tofauti za Instagram zinazoambatana na ujumbe mtamu.
Well, a day after he was remanded for more than two months until February 13, 2020, Jowie deleted most of the posts on his Instagram leaving only 22.
Kweli, siku moja baada ya kurudishwa rumande kwa zaidi ya miezi miwili hadi Februari 13, 2020, Jowie alifuta picha nyingi kule Instagram na kubakisha 22 pekee.
Alifuta pia picha alizopiga na Maribe na rafikiye wa dhati Joe Muchiri.
Zifuatazo ni baadhi ya picha alizofuta,
Maribe pia alifuta picha za mpenziwe wa zamani kutoka kwa mtandao wake wa Instagram pamoja na sherehe yao ya kuchumbiana.