logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mkewe Bahati , Diana Marua afunguka maisha ya ulevi

Mkewe Bahati , Diana Marua afunguka maisha ya ulevi

image
na

Burudani02 October 2020 - 04:31
Screenshot_from_2019_12_20_16_26_21__1576848403_98685
Mkewe Bahati Diana Marua amefunguka kuhusu tofauti ya maisha yanayozingira uraibu wa kwenda densi klabu na ndoa.

Akiwajibu baadhi ya mashabiki waliohoji kuwa bado anayakosa sana maisha ya klabu na kujiburudisha, Marua amesema kuwa alishachoka na maisha hayo na kuwa sasa anachokizingatia zidi ni maisha ya ndoa.

https://www.instagram.com/p/B6NUaLIgrkv/

“Hebu niwaambie kuwa hayo yote nishafanya. Nilifanya yote hayo. Hiyo parte after parte nishachoka. Yaani I served my life a good one mpaka sahii mimi hukaa chini nauliza leo ni Friday watu wako dunda? Watu wako tu huko wanashake their bum bum and doing other stuff. Sina muda huo, kwa sasa mimi ni mama wa watoto watatu na nishatulia. Nadhani nishafanya hayo yote na niko poa na jinsi nilivyo sasa...' Alisema Diana.

Haya yanajiri baada ya kufunguka kuwa kabla ampate Bahati, aliishi maisha ya ulevi na kwenda klabu.

Kulingana na Diana, Bahati alimvuta na kumleta kwa Mungu na hapo akaacha ulevi.

“Niliheshimu sana Bahati sana na nikijua kuwa naenda kumwona Bahati, ningetafuna PKs nyingi kuficha harufu ya pombe. Alikuwa anajua tu nimelewa kidogo japo nilijitahidi kuiyeyusha hali...' Alisema Marua katika mahojiano ya awali.

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved