logo

NOW ON AIR

Listen in Live

MKONO WA SHERIA :Ibrahim Akasha  Ahukumia miaka 23 Jela nchini Marekani

MKONO WA SHERIA :Ibrahim Akasha  Ahukumia miaka 23 Jela nchini Marekani

image
na

Burudani02 October 2020 - 04:40
Mwisho umetimia kwa familia ya ulanguzi wa dawa za kulevya ya Akasha baada ya mahakama nchini Marekani kumhukumu Ibrahim Akasha kifungu cha miaka 23 jela . Jaji wa Marekani  Victor Marrero  alimpa hukumu hiyo Ibrahim katika  korti ya  Manhattan  baada ya kuahirisha kikao cha kumhukumu mara mbili mwaka jana .

Mwanzoni ,hukumu hiyo ilifaa kutolewa  Novemba mwaka jana  kabla ya kusongeshwa  hadi disemba tarehe sita ,kisha tena ikasongeshwa hadi  januari tarehe 10 mwaka huu .Ibrahim amekuwa katika seli moja huko New York  kwa miaka mitatu akingoja hukumu dhidi yake  baada ya kuhamishwa hadi Amerika kutoka Mombasa januari mwaka wa 2017 .

Mnamo Oktoba mwaka wa 2018  Ibrahim na kakake mkubwa  Baktash  walikiri mashtaka dhidi yao katika mahakama ya Manhattan kwa kupanga njama ya kusafirisha dawa za kulevya za heroin  na  methamphetamine,  kubeba bunduki za rashasha  na vifaa vya kusababisha uharobifu  , makosa ya ulanguzi wa dawa za kulevya,kuwapa hongo maafisa wa Kenya ili kukwepa kuwajibikia uhalifu wao na kuzuia haki  kwa lengo la kuepuka kusafirishwa hadi marekani kujibu mashtaka dhidi yao. Jaji huyo mmoja ndiye aliyemhukumu Baktash kifungu cha miaka 25 jela agosti mwaka jana .


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved