logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Rais Uhuru Kenyatta amemuomboleza Jaji mstaafu Daniel Aganyanya

Rais Uhuru Kenyatta amemuomboleza Jaji mstaafu Daniel Aganyanya

image
na

Michezo02 October 2020 - 04:44
Daniel Aganyanya

Rais Uhuru Kenyatta amemuomboleza Jaji mstaafu Daniel Aganyanya akisema alikuwa mzalendo mashuhuri aliyethamini utawala wa sheria.

Katika risala yake kwa jamaa, ndugu na marafiki wa Jaji Aganyanya, aliyefariki akiwa na umri wa miaka 82 baada ya kuugua mshtuko wa moyo, Rais alisema jaji huyo wa zamani alikuwa shupavu katika vita dhidi ya ufisadi aliyepinga uovu huo hadharani.

“Jaji mstaafu Aganyanya ni mwanasheria aliyethamini uhuru wa mawazo. Alitetea bila uoga utawala wa sheria na aliamini uhuru wa kujisimamia kwa asasi za serikali hasa uhuru wa mahakama,” kasema Rais.

Huku akiongeza kwamba: “Justice Aganyanya atakumbukwa kama mwanasheria mwadilifu ambaye alisimamia alichoamini ni chema kwa nchi yake. Na akiwa Jaji, alikuwa mtu wa kuheshimika na kielelezo chema ambaye aliacha mfano bora katika sekta ya sheria.”

Rais Kenyatta alisema amehuzunishwa mno na kifo cha Jaji Aganyanya na akamuomba Mwenyezi Mungu kuifariji familia yake wakati huu mgumu wa maombolezo.

“Naomba Mwenyezi Mungu awafariji na kuwapa nguvu  wakati huu wa majonzi. Nawaombea,” kasema Rais.

Marehemu Aganyanya alistaafu kutoka Idara ya Mahakama ambako alihudumu katika Mahakama ya Rufaa mnamo mwaka wa 2012 baada ya kutimiza miaka ya kustaafu ya  umri wa miaka 74.

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved