logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Familia ya mzee Moi:Watoto wa Rais Moi

Familia ya mzee Moi:Watoto wa Rais Moi

image
na

Habari02 October 2020 - 04:53
baba moi
Marehemu Rais mtaafu Daniel Moi alikuwa na watoto wanane wakiwemo pacha.  Mmoja wa wanawe wa kiume alijiunga na jeshi, mwngine alikuwa dereva mashuhuri wa mbio za magari  ilhali mwingine alijipata katika vichwa vya habari katika kesi yake ya talaka.

Familia hiyo pia ina wanasiasa lakini sio wenye  jazba ya kuvutia kama Marehemu baba yao. Moi  alimuoa Lena Moi, binti ya  mkulima mmoja mashUhuri na mhubiri huko Eldama Ravine  Paul Bomet mwaka wa 1950. Pamoja walipata watoto wanane –wavulana watano na wasichana watatu. Lena  alikuwa mwalimu lakini baadaye akaamua kusalia nyumbani kuwatunza wanawake na pia kumsaidia Moi aweze kuzingatia taaluma yake katika siasa .

Mtoto wa Moi anayejulikana sana ni  kitinda mimba seneta wa Baringo Gideon Moi aliyezaliwa mwaka wa 1964. Gideon alionekana kupendwa sana na Mzee Moi  na amechukua jukumu la kuwa msemaji wa Familia kubwa ya Moi. Kifungua mimba wa Moi ni msichana  Jenniffer Chemutai Kositany aliyezaliwa mwaka wa 1953 na alisomea katika shule ya   Kenya High  kabla ya kuelekea marekani kwa masomo ya chuo kikuu. Amesalia kuendeleza maisha ya kibinafsi bila kuangaziwa sana. Jennifer  ni mjane na aliolewa  na Stephen Kositany  ambaye alitokea familia maarufu kisiasa huko Nandi na aliaga dunia katika ajali ya barabarani .

Marehemu Stephen  ni kakake mbunge wa sasa wa Soy Caleb Kositany . Jonathan Moi aliyekuwa akipenda sana kuendesha magari ya mashindano  ndiye mtoto wa pili na mvulana mkubwa wa Mzee Moi  na aliaga dunia aprili mwaka wa 2019  baada ya kuugua saratani kwa muda mrefu .inaripotiwa alikuwa karibu sana na mamake ,Lena kuliko alivyokuwa na mzee Moi .John Mark, mwanawe wa tatu wa mzee Moi  ndiye ambaye hafahamiki sana na wengi .Alizaliwa mwaka wa 1958 na kaishi marekani kwa muda akisoma lakini akarejea nchini kabla ya kutamatisha masomo yake.  Wanawe wengine wa Moi ni mbunge wa sasa wa Rongai  Raymond Moi na mapacha  Philip na Doris waliozaliwa mwaka wa 1962.

Philip ni meja mstaafu  wa jeshi  na alikuwa miongoni mwa wakenya wachache walioanzisha mchezo wa  mbio za  farasi.  Amepata  kibarua kigumu kortini katika kesi yake ya talaka  ambapo  mke wanayetengana naye  Rosana Pluda  alitaka kulipwa shilingi milioni 90 za matumizi kila mwezi .

Doris,  kwa upande wake amedumisha maisha ya faraghani lakini anahudumu katika bodi kadhaa za shule zinazohusishwa na mzee Moi . Alisomea shule ya msingi ya Nairobi, Limuru Girls na baadaye Imani School Thika kabla ya kwenda kuishi Australia kwa muda.  Doris pia ni mjane na aliolewa na  rafikiye kakake Jonathan katika mbio za magari Simon Choge .

Choge aliaga dunia katika ajali ya barabarani .June, bintiye mdogo Moi ni mtoto wa kulelewa. Kama Gideon alikuwa amependwa sana na Mzee Moi .  Alisomea Nairobi Primary, Kenya High School  kisha akaelekea chuo kikuu Canada. Ni mfanyibiashara mashuhuri.

Mzee Moi  na Mama Lena walitengana mwaka wa 1974 na kisha kutalakiana mwaka wa 1979. Rais mstaafu hakuoa tena . Lena aliishi Rongai kwa maisha tulivu  alikofariki mwaka wa 2004. Licha ya kila mmoja kuishi kivyake kwa miaka 30, alizikwa katika shamba kubwa la Moi la Kabarak .


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved