logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Majibu Nayo! Tazama jinsi Raila Odinga Junior alivyorusha ‘kombora’ twitter

Majibu Nayo! Tazama jinsi Raila Odinga Junior alivyorusha ‘kombora’ twitter

image
na

Burudani02 October 2020 - 05:06
Mwanawe kiongozi wa ODM Raila Odinga Junior  jana amempiga mmoja wa watumizi wa twitter  kumbo kali sana pale twitter alipojaribu kutilia doa kiwango cha masomo yake . Jamaa huyo Joseph Omondi alijutia mbona alianzisha vita hivyo na Junior kwani jibu lake sio lililotarajiwa .

Wengi wa wanaotumia twitter wanbafahamu kwamba mfalame wa majibu makali huwa   wakili Miguna Miguna lakini huenda anapata ushindani kutoka kwa Raila Junior . Hata hivyo wengi wa waliofuatilia majibizano hayo kati ya Omondi na Raila Junior walionekana kughadhabishwa na jibu ambalo Junior alilitoa wakisema kama mtoto wa  Raila Odinga ,alifaa kuonyesha  ustaarabu kidogo mtandaoni .

https://twitter.com/Railajunior/status/1228883044863479809

Katika majibizano hayo Omondi alikuwa akieleza kwamba mwanawe Naibu wa rais  June Ruto ana kisomo zaidi ya Raila Junior na hivyo basi anastahili kushikilia nafasi  anayohudumu  kama mwakilishi wa balozi huko Poland .Hata hivyo majibu ya RailaJunior yalimuacha kila mtu kinywa wazi .

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved