logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Diamond yuko Single! Asema dadake Queen Darleen

Diamond yuko Single! Asema dadake Queen Darleen

image
na

Habari02 October 2020 - 05:55
Msanii wa Bongo Diamond Platinumz yuko Single na wanadada wanafaa kukumbuka hilo wakati wote. Hayo  yamesemwa na dadake msanii huyo Queen Darleen ambaye amesema kakake bado ni mtanashati na hivyo basi hafai kujifungia.

https://www.instagram.com/p/B-Jk3uRpUSn/

Queen aliyasema hayo katika ujumbe  alioambatanisha na picha ya kakake katika akaunti yake ya instagram. Huenda sasa ni rasmi kwamba  Simba kweli kaachana na Tanasha Donna kwa sababu dadake anawafungilia wanadada wengine milango katika maisha ya kaka yake.

Katika posti hi ya Insta, dadake mwingine wa Diamond, Esma naye alicheka kwa bezo akisema kwamba huenda akina dada wanamuogopa Kaka yao. Huenda familia ya Diamond ipo nyuma yake kuhusu maamuzi anayofanya ya kuwatema vipusa wote wanaoingia katika maisha yake. Huku wanadada walioathirika wakilalama, dada zake na mamake wameonekana kulichukulia suala zima kama sarakasi na drama!

Mhariri: Davis Ojiambo


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved