logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Vile Diamond alifichuwa kuwa producer Ayo Lizer ana virusi vya corona

Vile Diamond alifichuwa kuwa producer Ayo Lizer ana virusi vya corona

image
na

Habari02 October 2020 - 09:39
Diamond Platnumz amefichuwa vile producer  wake Ayo Lizer ameambukizwa na virusi ya corona, yanajiri haya huku  meneja wao  Sallam SK  Mendez akipatikana na virusi vya corona mnamo Machi, 19.

Diamond alitangaza haya katika video moja alipokuwa akizungumza na mhudumu wa afya na kumuuliza jinsi walivyokuwa wanaendelea na matibabu.

" Kwa mfano kama vile Lizer amepatikana na virusi vya corona, lakini anaonekana mwenye afya na hana shida yeyote itachukua muda gani yeye kupona kabisa na kurudi nyumbani."  Diamond Alizungumza.

Akijibu swali la msanii wa bongo alikuwa na haya ya kusema;

"Kirusi cha corona kinaweza kuwa katika mwili wako, mbali uonekane mwenye afya, lakini unaweza kuambukiza waliokaribu na wewe

Corona ikiisha katika mwili wako ukienda kupimwa tena matokeo yake huwa yanaonyesha kuwa huna kirusi hicho

Baada ya kupimwa huwa unangoja kwa muda wa siku saba kisha unapima tena, kwa hivyo katika kipindi hiki cha karantini kwa siku kumi na nne unapaswa kupimwa mara mbili.

Ukipatikana hauna kirusi hicho hivyo basi utaruhusiwa kwenda nyumbani." Alieleza.

Ni video ambayo ilisambaa sana katika mtandao wa kijamii, licha ya hayo mzalishaji Lizer hajajitokeza na kuzungumzia hali yake ya afya.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved