Kifo chake katika hali ya kutatanisha akiwa nyumbani kwake Sinza, Dar es Salaam bado kinajadiliwa hadi leo hasa siku hii ambapo kumbukizi ya kifo chake inaadhimishwa. Kanumba alipata umaarufu na kuibuka kama muigizaji balozi wa filamu za Kiswahili katika Tanzania na afrika mashariki.Wakati wa mazishi yake, maelefu ya watu waliyahudhuria na hata rais Jakaya kikwete aliahirisha safari yake nje ya nchi ili kwenda kumzika msanii huyo. Mamia ya watu pia walisafiri kutoka maeneo ya Bunia na Kisangani,mkatika Jamhuri ya DRC kwenda kumzika Kanumba .
Awali ilidaiwa Kanumba alifariki baada ya kugombaa na muigizaji mwenzake Elizabeth Michael aka Lulu . Lulu baadaye alihukumiwa jela kwa mwaka mmoja na kuachiliwa. Alidai Kanumba alijaribu kumshambulia kwa panga na kumfanya kuanguka hadi akazirai.B aadaye alipopata fahamu alitoroka kuokoa maisha yake lakini akaarifiwa kwamba Kanumba alikuwa ameaga dunia .
Steven Kanumba alizaliwa mwaka 1984 na anatajwa kuwa ni mmoja wa waigizaji walioitambulisha na kuikuza sanaa hiyo ndani na nje ya mipaka ya Tanzania. Maudhui ya filamu zake na umaarufu wake ulimfanya kupendwa kote Afrika, na kisa chake cha kupanda hadi kilele cha utajiri kutoka familia maskini pia kilikuwa kama jambo la kuwapa wengi matumaini .